• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU MKOANI RUVUMA YAFANIKIWA KUFUATILIA MIRADI YA THAMANI YA BIL. 6.3

Tarehe ya kuwekwa: November 30th, 2022

Kwa mujibu wa kifungu cha 7 cha sheria ya kuzuia na kupamabana na Rushwa Na.11 ya mwaka 2007, TAKUKURU inayo majukumu makuu mataTu ambayo ni pamoja kuelimisha jamii juu ya Rushwa na madhara yake, kufanya uchambuzi wa Mfumo kwenye taasis za umma na sekta binafsi pamoja na kufanya uchunguzi na kufikisha watuhumiwa makamani kwa kibali cha Mkurugenzi wa mashtaka (DPP) baada ya uchunguzi kukamilika.

Tamko hilo limetolewa jana  tarehe 29/11/2022  na Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Janeth  Haule  katika kikao cha waandishi wa Habari kilichofanyika  ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma kwa  Lengo la kuhabarisha umma  juu ya  ufuatiliaji wa miradi inayotekelezwa na Taasis  na thamani ya fedha iliyotolewa.

Janeth alisema TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma  katika kipindi cha Julai hadi Septemba wamefanikiwa kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo yenye thamani ya zaidi Bil. 6,359,392,899.80 katika miradi ya ujenzi wa barabara Manispaa na Wilaya ya Mbinga ya thamani 5,764,392,899.80 na nyumba za watumishi Wilaya ya Tunduru na Nyasa zenye thamani ya Mil. 125,000,000, ujenzi wa shule mpya ya Sekondari Wilaya ya Tunduru wenye thamani ya 470,000,000/=.

Aliongeza kuwa  TAKUKURU Mkoa Ruvuma unaendelea na jukumu la kuelimisha umma kwa kuyafikia makundi mbalimbali ya jamii kwa lengo kuwajengea uelewa wa madhara ya Rushwa ambapo kupitia uelimishaji huo wameweza kuwafikia wananchi kupitia semina 11 zilizoandaliwa, klabu za wapinga Rushwa 79 za shule za msingi na Sekondari, mikutano ya hadhara 62, makala 3 pamoja na taarifa kwa umma moja. “ Janeth Alibainisha”.

Alisema TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma katika kipindi cha Julai hadi Septemba 2022 wameweza kuteleza majukumu ya uchunguzi na kufanikiwa kupokea taarifa mpya  48 za malalamiko kati ya taarifa hizo taarifa 24 zilihusu Rushwa na uchunguzi unaendelea, pia taarifa 24 hazikuhusu Rushwa hivyo walalamikaji walishauriwa kupata msaada kwenye taasis husika.

Aidha katika taarifa za malalamiko zilizopokelewa  zilihusu Serikali za Mitaa 10, Ardhi 9, Afya 7, Elimu 4, Halmshauri 3, Polisi 3, Mahakama 2, Ustawi wa jamii 2, Siasa 2, na sekta nyingine za fedha, kilimo, mifugo, TASAFna maji ambazo kila moja zina lalamiko mojamoja.

Alibainisha kuwa kuanzia Oktoba hadi Disemba TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma wamejipanga kuendelea kuelimisha wananchi juu ya Rushwa na madhara yake katika usimamizi wa miradi ya maendeleo kwa lengo la kuwawezesha wananchi kupata uelewa na kusimamia utekelezaji wa miradi  kwa karibu na weledi wa hali ya juu. “Alisisitiza.” 

IMETOLEWA NA;

AMINA PILLY

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa