• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU Ruvuma yamfikisha mahakamani Mchumi wa Halmashauri

Tarehe ya kuwekwa: February 8th, 2019

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU mkoani Ruvuma imemfikisha mahakamani Mchumi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Sydeny Mpangala  kwa makosa  kutumia nyaraka kumdanganya mwajiri wake na kujipatia zaidi ya shilingi milioni 1.8.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa umma na Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Owen Jasson, Februari,7 mwaka huu TAKUKURU ilimfikisha mtuhumiwa huyo katika mahakama ya Wilaya ya Mbinga akikabiliwa na makosa mawili.

Jasson ameyataja makosa hayo kuwa ni kutumia nyaraka kumdanganya mwajiri kinyume na kifungu cha  22 cha sheria ya  Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11/2007 na kuisababishia hasara serikali  kinyume na aya ya 10(1) ya jedwali la kwanza na kifungu cha 57(1) na 60(2) vya sheria ya uhujumu uchumi sura ya 200 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Kulingana na Kaimu Mkuu wa TAKUKURU,Machi 25,2017,TAKUKURU ilipokea taarifa kuwa Sydney Mpangala alitumia nyaraka kumdanganya mwajiri na kujipatia kiasi cha sh.1,803,510 na kwamba nyaraka hizo zilizonesha kuwa fedha hizo zilitumika kununulia vifaa mbalimbali visivyokuwa vya viwandani kwa ajili ya ujenzi wa kibanda cha Mlinzi kwenye nyumba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo iliyopo eneo la Kipika mjini Mbinga.

“Baada ya kupokea taarifa hiyo uchunguzi ulifanyika na kukusanya ushahidi uliothibitisha kuwa mtuhumiwa alitenda makosa ya udanganyifu na kuisababishia hasara serikali,hivyo tarehe 07/02/2019,mtuhumiwa alifikishwa kwenye mahakama ya Wilaya ya Mbinga na kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi namba moja ya mwaka 2019’’,alisema Jasson.

Kesi hiyo ilisomwa na Wakili wa Serikali Gregory Chisauche mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mbinga Aziza Hassan Mbadjo.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Februari,8,2019

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa