• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU Ruvuma yamfikisha Mahakamani Mtendaji wa Kata kwa Rushwa

Tarehe ya kuwekwa: May 18th, 2019

TAASISI ya Kuzuia Na Kapambana na Rushwa TAKUKURU mkoani Ruvuma imemfikisha katika Mahakama ya Wilaya ya Mbinga Afisa Mtendaji wa Kata ya Linda Cosmas Nyoni akituhumiwa kwa makosa ya kuomba na kupokea fedha kwa njia ya rushwa.

Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa na Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Owen Jasson,Mtuhumiwa amefanya kosa  kinyume na kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya mwaka 2007.

Jasson amesema mnamo Agosti 3,2018,ofisi ya TAKUKURU  Wilaya ya Mbinga ilipokea taarifa kuwa Cosmas Nyoni kwa njia za rushwa  Juni 29,2018 aliomba fedha kiasi cha shilingi 550,000 kutoka kwa Zacharia Komba ili asiweze kumchukulia hatua na  kumpelekea watu wa upekuzi nyumbani kwake ili kumpekua kwa makosa ya kujihusisha na ununuzi holela wa kahawa iliyopigwa marufuku ya magoma.

“Siku hiyo Mtuhumiwa alipokea fedha kiasi cha shilingi 100,000 ikiwa ni sehemu ya fedha alizoomba na siku ya Julai 4,2018 alipokea  tena fedha nyingine kiasi cha shilingi 250,000,pia ikiwa ni sehemu ya fedha alizokuwa ameomba’’,alisema Jasson.

Amesema baada ya kupokea taarifa hiyo,uchunguzi ulifanyika ambapo ilithibitika kwamba ni kweli Mtuhumiwa ametenda makosa ya rushwa  ambapo Mei 17 mwaka huu,Mtuhumiwa amefikishwa  kwenye Mahakama ya Wilaya ya Mbinga na kufunguliwa kesi ya Jinai Namba 41 ya mwaka 2019.

Kulingana na Naibu Mkuu wa TAKUKURU,Kesi hiyo imesomwa na Wakili wa Serikali Chali Kadeghe mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mbinga Aziza Hassan Mbadjo.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Serikalini

Mei 17,2019

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa