• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU Ruvuma yaokoa milioni 53

Tarehe ya kuwekwa: August 2nd, 2018

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma imeokoa kiasi cha Zaidi ya shilingi milioni 53 ambazo zingetumika kama mishahara hewa katika sekta ya afya,elimu na TAMISEMI.

Akitoa taarifa ya utendaji kazi wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma kwa wanahabari katika kipindi cha kuanzia Julai 2017 hadi Juni 2018,Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yustina Chagaka amesema kati ya fedha zilizookolewa katika sekta ya afya pekee zimeokolewa Zaidi ya shilingi milioni 44.

Kulingana na Chagaka katika sekta ya elimu zimeokolewa shilingi milioni tatu na TAMISEMI Zaidi ya shilingi milioni tano na kwamba fedha hizo zimerejeshwa serikalini na kuongeza kuwa shilingi milioni sita zimerejeshwa kwenye kikundi husika ambako zilichukuliwa kinyume cha utaratibu.

“Katika kipindi hicho majalada ya uchunguzi 45 yalifunguliwa na majalada ya uchunguzi 22 yalikamilika kuchunguzwa na kutumwa katika Mamlaka za Juu kwa mapitio,majalada yaliopelekwa kwa Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP) kuombewa vibali vya mashtaka ni tisa na ambayo tayari yamepatiwa  kibali cha mashtaka ni manne’’,anasisitiza Chagaka.

Kulingana na Mkuu huyo wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma,katika kipindi hicho TAKUKURU imepokea taarifa 298 kutoka kwa wananchi kupitia vyanzo mbalimbali ambapo amezitaja Idara zinazoongoza kulalamikiwa kuwa ni serikali za Mitaa(Ofisi ya wilaya,kata,vijiji na mitaa taarifa 70.

Idara nyingine ni Ardhi taarifa 53,Polisi 30,Mahakama 26,Kilimo 23,Elimu 19,Ujenzi 13,Afya 11,Vyama vya siasa 11,Hifadhi ya Jamii 4,Fedha 4 na Maliasili,NIDA na sekta binafsi kila mmoja imepokea malalamiko matatu.

“TAKUKURU inaendelea kuwaasa wananchi wote kushirikiana nasi katika mapambano haya kwa kukataa kujihusisha na vitendo vya vya Rushwa,kukemea vitendo vya rushwa na kutoa taarifa za vitendo vya rushwa katika ofisi za TAKUKURU’’,anasisitiza Chagaka.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Agosti 2,2018

Mawasiliano albano.midelo@gmail.com,simu 0784765917

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa