• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU Ruvuma yaokoa Shilingi Milioni 90

Tarehe ya kuwekwa: May 5th, 2017

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa  TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma,katika kipindi cha kuanzia Julai 2016 hadi Machi 2017 imeokoa kiasi cha zaidi ya sh. 91 ambayo yalikuwa ni malipo hewa.

 Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yusta Chagaka amewaambia wanahabari ofisini kwake mjini Songea kuwa  kati ya fedha hizo katika sekta ya elimu ziliokolewa zaidi ya sh.milioni 61 na sekta ya kilimo zaidi ya sh.milioni 2.2 kama mishahara hewa.

Chagaka anabainisha zaidi kuwa katika sekta ya ujenzi kiasi cha sh.milioni 28.5 ziliokolewa, na kwamba kiasi hicho cha fedha kililipwa kwa mkandarasi katika mradi wa ujenzi wa barabara ya Mpitimbi B hadi Mbinga Mhalule katika Halmashauri ya Songea kwa kazi ambazo hazikufanyika.

Amesema TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma katika kipindi hicho  imepokea taarifa za malalamiko 173 kutoka kwa wananchi kupitia vyanzo mbalimbali.

Anazitaja idara zinazoongoza kulalamikiwa kuwa ni malalamiko 40 toka TAMISEMI,Elimu malalamiko 26, Kilimo 21, Afya 18, Ujenzi 17, Ardhi 16, Mahakama 14, Maji 10, Polisi 9 na Watu binafsi mawili.

Katika kuendelea kutekeleza jukumu la kushirikisha na kuelimisha jamii dhidi ya Rushwa Mkuu wa  TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma  anasema ofisi yake Imefanya Semina 53, Mikutano ya hadhara 45 na kuanzisha Klabu 51 za wapinga rushwa katika shule za msingi, sekondari na vyuo zimeelimishwa na kuimarishwa.

Chagaka anasema katika kipindi hicho miradi ya maendeleo 12 inayohusu ujenzi wa miundombinu ya Afya, Elimu, Maji, Kilimo na mifugo yenye thamani ya zaidi ya  sh.bilioni 3.5 ilikaguliwa.

Anasema baadhi ya miradi hiyo ilikuwa na viashiria vya ubadhirifu hivyo uchunguzi wa matumizi ya fedha ya miradi hiyo unaendelea na upo katika hatua mbalimbali za uchunguzi.

Anaitaja mikakati ya TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma katika kumaliza kero kwa wananchi ni kufuatilia fedha za miradi ya maendeleo kama zinatumika ipasavyo,kuendelea kufanya tafiti ndogo katika idara mabalimbali za Umma zinazolalamikiwa ili kubaini mianya ya rushwa na kupendekeza njia madhubuti za kuziba mianya hiyo kwa manufaa ya wananchi.

Mikakati mingine ni Kufanya warsha zinazohusisha wadau mbalimbali na idara zinazolalamikiwa ili kuweka mikakati ya pamoja ya kuziba na kuiondoa kabisa mianya ya rushwa katika idara husika.

Anasema TAKUKURU itaendelea kufanya uchunguzi kwa weledi ili kuhakikisha malalamiko yote yanachunguzwa ipasavyo na  watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa kuchukuliwa hatua za kisheria dhidi yao.

Anasisitiza TAKUKURU inajenga mahusiano madhubuti na wadau mbalimbali ili kuhakikisha wanashiriki kikamilifu na kwa dhati katika mapambano dhidi ya rushwa na kuendelea kuelimisha wananchi katika ngazi mbalimbali juu ya madhara ya rushwa ili waichukie rushwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa