• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU Ruvuma yatoa Ripoti ya Utendajikazi ya kuanzia Aprili hadi Juni 2019

Tarehe ya kuwekwa: July 18th, 2019

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU mkoani Ruvuma imefanya uchambuzi wa mifumo mitatu ili kubaini mianya ya rushwa katika sekta ya Elimu katika usimamizi wa mitihani ya kitaifa.

Mkuu wa TAKUKURU mkoani Ruvuma Yustina Chagaka akitoa taarifa ya utendajikazi wa TAKUKURU katika kipindi cha miezi mitatu kuanzia Aprili hadi Juni 2019 kwa wanahabari mjini Songea ,amesema mianya hiyo imechunguzwa katika Halmashauri za Manispaa ya Songea,Halmashauri ya Wilaya ya Songea na Madaba.

Amesema katika kipindi hoicho TAKUKURU ilifanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa maazimio ya warsha ya wadau kuhusu mfumo wa ukusanyaji wa mapato yatokanayo na ujazaji fomu za afya kwa wanafunzi wanaoanza masomo ya sekondari katika Halmashauri za Mji Mbinga na kuokoa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 22.

Kamanda wa TAKUKURU mkoani Ruvuma Christina Chakaga ametoa wito kwa Halmashauri kutoa elimu ya sheria kwa mabaraza ya ardhi ya Kata.

Kuhusu mabaraza ya ardhi Chagaka amesema mabaraza ya ardhi ya Kata  yanafanya kazi za  kisheria,wakati hawana elimu ya sheria jambo  linalosababisha kuongezeka kwa vitendo vya rushwa katika Idara ya ardhi wakati wa kutatua migogoro baina ya mlalamikaji na mlalamikiwa.

“Katika kipindi cha miezi mitatu TAKUKURU mkoani Ruvuma imepokea taarifa  za malalamiko ya rushwa 63 toka vyanzo mbalimbali ambapo kati ya malalamiko hayo idara ya ardhi inaongoza kwa kulalamikiwa kwa malalamiko  17’’,alisema.

Ameitaja Idara inayofuatia kwa kulalamikiwa kuwa ni idara ya elimu yenye malalmiko 10 na ya mwisho kulalamikiwa ni taasisi za kifedha zenye malalamiko mawili.

Aidha TAKUKURU Ruvuma imefanya ufutiliaji wa zaidi ya shilingi bilioni 14 ambazo zimetolewa na serikali kwa ujenzi wa miradi ya miundo mbinu ya ujenzi, maji,afya,elimu na barabara nakubaini dosari ndogondogo ambazo zimeshatolewa ushauri wa wanamna ya kurekebisha  dosari hizo.

Akizungumzia kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajia kufanyika nchini baadaye mwaka huu, Chakaga amewataka wagombea na wapiga kura kujiepusha na vitendo vya rushwa ambavyo vitawasababishia matatizo ya kuchukuliwa hatua za kisheria kulingana na sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007 ya kuongoza vita dhidi ya rushwa na ufisadi nchini.

TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma imeendelea kutekeleza matakwa ya Sheria inayoongoza majukumu matatu  ambayo ni kuzuia rushwa,kuelimisha umma na kuchunguza tuhuma za rushwa na kushitaki watuhumiwa.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Julai 20,2019

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa