• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TANCOAL yakumbushwa kulipa deni la madini ya Makaa ya mawe ya Ngaka

Tarehe ya kuwekwa: November 16th, 2019

Waziri wa Madini Doto Biteko amewakumbusha Viongozi wa Kampuni ya TANCOAL kuanza kulipa deni lao la kiasi cha Dola za Kimarekani 10,408,798 ambalo Kampuni hiyo inadaiwa na Serikali kwa kipindi cha Septemba 2011 hadi Septemba 2019. Kauli huyo ameitoa leo Novemba 15, 2019 wakati alipokutana na Viongozi wa Kampuni ya TANCOAL inayojishughulisha na uzalishaji wa Makaa ya Mawe katika Mgodi wa Ngaka Mkoani Ruvuma.

Kikao hicho kimefanyika katika Ofisi za Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) Jijini Dodoma na kuhudhuriwa pia na baadhi ya Viongozi Waandamizi wa Wizara wakiwemo Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Augustine Ollal, Mkurugenzi wa Huduma za Sheria Edwin Igenge, Mjiolojia wa Wizara ya Madini Neema Msinde na Mjiolojia Kutoka Tume ya Madini Ezekiel Seni. 

Aidha, Waziri Biteko ameisisitiza Kampuni hiyo kuzingatia suala la ushirikishwaji wa Nchi na Wananchi (Local Content), katika shughuli zao na kutoa mfano wa Kampuni ya Shanta Gold Mine kuwa ina asilimia 100 ya Watanzania ambao wanafanya kazi katika mgodi huo ukiwemo Mgodi wa Geita Gold Mine ambao una asilimia 97 za Watanzania ambao wanafanya kazi katika mgodi huo.

Hata hivyo, Waziri Biteko amewakaribisha wawekazaji hao na kuwaeleza kuwa Serikali inataka wawekezaji wake wapate faida na walipe kodi kwa Serikali. 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kampuni ya TANCOAL Graeme Robertson ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa hatua inazozichukuwa za kukuza sekta ya Viwanda ambavyo kwa asilimia kubwa huwa zinatumia Nishati ya Makaa ya Mawe katika shughuli za uzalishaji.

Nao, Viongozi wa Kampuni ya TANCOAL wamemshukuru Waziri Biteko kwa maelekezo na ushauri suala ambalo wanaamini itawasaidia katika kupeleka mbele maendeleo la Kampuni hiyo.

Pia, ameongeza kwamba mahusiano mazuri na Serikali ndilo jambo la msingi linaloweza kusaidia katika kukuza uchumi Nchini na Duniani kote, sababu ambayo ilipelekea kukutana na Waziri wa Madini ili kuzunguza masula yatakayo saidia kuboresha uzalishaji wa Makaa ya Mawe katika kampuni hiyo.

Robertson amesema kuwa Kampuni ya TANCOAL ina masoko ndani na nje nchi, ambapo wanunuzi wakubwa wa Makaa ya Mawe nchini ni makampuni ya Saruji, Vigae na viwanda mbalimbali, pia Kampuni husika inasafirisha Makaa ya Mawe kwenda nchi jirani za Kenya, Uganda, Rwanda na Malawi.




“Inchi ya Indonesia inapata pato kubwa kutokana na usafirishaji wa Makaa ya Mawe hivyo naamini hata Tanzania inaweza ikapandisha mapato yake kupitia usafirishaji wa Makaa ya Mawe,” amesema Robertson.

Ameongeza kuwa nchi ya Malawi pia ina kiwango kikubwa cha Makaa ya Mawe isipokuwa tatizo lipo kwenye uchimbaji wake ambapo ni vigumu sana kuyachimba kutokana na mazingira magumu yalipo Makaa hayo ukilinganisha na Makaa yaliyopo Tanzania.




Pia, Robertson amesema Kampuni hiyo inampango wa kuvitumia Vyuo Vikuu vya Tanzania ili kuhakikisha wafanyakazi wa kampuni hiyo wanakuwa na ujuzi wa kutosha katika suala la uzalisha na usafishaji wa Makaa ya Mawe.



 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA July 08, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 July 04, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Dkt. Samia Awasili Ruvuma.

    July 30, 2025
  • Mhe. Jenista Waziri wa Afya; Serikali yapambana kupunguza Maambukizi Mapya ya Virus vya Homa ya INI.

    July 29, 2025
  • Songea MC Yadhamiria Kuboresha Lishe na Kuondoa Udumavu

    July 25, 2025
  • Songea MC - Yaibuka na Ushindi katika Mechi ya Kirafiki Dhidi ya Namtumbo.

    July 24, 2025
  • Tazama zote

Video

Dkt. Samia Akiwasili Songea
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa