• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TCRA CCC YATOA SEMINA KWA WATUMIAJI WA HUDUMA YA MAWASILIANO.

Tarehe ya kuwekwa: February 1st, 2023

Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano (TCRA CCC) limeanzishwa  kwa kifungu cha 40 cha Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Na. 12 ya mwaka 2003 kama ilivyorekebishwa mwaka 2017 ikiwa na majukumu ya kuwa kiungo  baina ya Watumiaji wa Huduma zinazosimamiwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Watoa Huduma, TCRA na Serikali.

Baraza hilo linatekeleza Mpango mkakati wa miaka mitano 2019/2020-2025/2026 wenye lengo la kiuboresha ustawi wa watumiaji na kuongeza uelewa wa masuala ya huduma bidhaa za mawasiliano  ni Dira ya Baraza ambalo ni chombo imara na cha kutegemewa katika kutetea haki na maslahi ya watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano pamoja na kuleta maelewano miongoni mwa wadau wa sekta ya Mawasiliano.

Hayo yamejili wakati wa semina ya kuelimisha na kuhamasisha Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano iliyoshirikisha makundi mbalimbali wakiwemo  Waheshimiwa Madiwani, Wenyeviti wa Mitaa, Wajasiliamali, Wanawake, Vijana, Mafundi Simu, Mawakala wa usajili laini za simu, wawakilishi wa NGO’S na viongozi wa dini kwa lengo la kuelimisha watumiaji,  kushauriana na kupokea maoni uliofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea tarehe 31 Januari 2023.

Katibu Mtendaji Baraza la Ushauri la watumiaji wa huduma za mawasiliano  TCRA CCC Bi Mary Shao Msuya  alisema  jukumu la kutunza miundombinu ya Mawasiliano ni la wananchi ambao ni  watumiaji na endapo utaona kuna dalili yoyote ya uhalifu unapaswa kutoa taarifa polisi kwa hatua zaidi.

Bi Msuya  alisema Mkutano huo ni mwendelezo wa utekelezaji wa majukumu ya baraza ambayo wamejipangia mwaka huu yenye  kuelimisha, kuhamasisha, kupokea maoni kutoka kwa watumiaji  na kuanzisha kamati katika  Mkoa wa Ruvuma ambayo  ni  kamati ya 18 kati ya hizo kamati 16 ni za Tanzania Bara na kamati mbili ni za Tanzania Visiwani.

Aliongeza kuwa Sekta hiyo ina changamoto nyingi ikiwemo na uelewa mdogo kwa watumiaji wa huduma za mawasiliano ikiwemo na kutumia simu zilizosajiliwa kwa jina la mtu mwingine na  kutuma picha zisizo na maadili.

Akibainisha   Wajibu wa Watumiaji wa huduma za Mawasiliano ni kutii sheria za nchi za matumizi halali ya huduma, kulipia huduma wanazozitumia, kuhifadhi mazingira na utunzaji wa mawasiliano, kuelewa huduma wanazopata, kuwa makini katika matumizi na kujilinda, kulalamika na kuwasilisha malalamiko kuhusiana na huduma na kutambua kasoro katika matumizi na utoaji wa taarifa.

Kwa upande wake Afisa kutoka sehemu inayoshughulikia masuala ya wateja na watumiaji TCRA  Sohela Mabeyo alisema hadi Septemba 2022 Tanzania jumla ya laini za simu 58,118,961, ambapo kwa Mkoa wa Ruvuma hadi kufikia June 2022 jumla ya laini 1,510,498, hadi kufikia june 2022 jumla ya watumiaji wa Internet 31,122,163, pia hadi kufikia juni 2022 akaunti za PESA  za mtandao ni 39,590,502.

Akibainisha makosa mbalimbali ya uvunjifu wa sheria ambayo ni pamoja na  kupiga picha zilizokinyume na maadili, kufanya biashara ya utapeli mtandaoni, kupigiwa simu na matapeli ambapo alisema namba ya huduma kwa Wateja ni 100 pekee ambapo amewataka watumiaji kutumia mitandao kwa uangalifu ili kuepuka uvunjaji wa  sheria. . “Alisisitiza.”

Alisema usipokee maelekezo kutoka namba yoyote isiyokuwa namba 100  kinyume na hapo  wengi huishia kutapeliwa ambapo alitoa maelekezo kuwa ikitokea umetapeliwa kwa njia ya simu tafadhali tumia namba 15040 ambayo utaingia kwenye uwanja wa ujumbe (SMS) utaandika neno UTAPELI kwa herufi kubwa na kama kuna ujumbe utaweka kisha utatuma 15040 hatimaye hiyo namba itafungiwa. “Mabeyo alisisitiza.” 


Kwa upande wa wadau waliohudhuria semina hiyo walitoa shukrani kwa Serikali kwa kutoa mafunzo hayo ambayo yamewasaidia katika kutambua matumizi bora ya huduma za mawasiliano.

 

Mwisho

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI..



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa