• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TFDA YAKAMATA MAFUTA YA ALBINO NA VYAKULA VIBOVU

Tarehe ya kuwekwa: October 11th, 2017

TFDA YAKAMATA MAFUTA YA ALBINO NA VYAKULA 

IDARA ya Afya katika Manispaa ya Songea kwa kushirikiana na watalaam wa Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) wamefanya operesheni katika maduka ya vipodozi katika mji wa Songea na kufanikiwa kukamata mafuta ya albino yakiuzwa kinyume cha sheria.

Mganga Mkuu wa Manispaa ya Songea Dk.Mameritha Basike amesema mafuta hayo yalikamatwa katika duka la Godluck Mranga ambayo alikuwa anauza shilingi 4500.

“Hairuhusiwi mafuta ya kupaka Albino aina ya sunblock cream UV40 kuwepo kwenye maduka ya vipodozi badala yake mafuta hayo yanaruhusiwa kuwepo kwenye maduka ya dawa (Pharmacy)’’,anasisitiza Dk.Basike.Amesema katika duka hilo pia vimekamatwa vyakula mbalimbali vilivyoharibika vikiwemo maziwa ya kopo 12 yenye thamani ya zaidi ya sh.200,000 na nyama ya kopo 20 zenye thamani ya sh.100,000.

Afisa Afya wa Manispaa ya Songea Vitalis Mkomela amesema mfanyabiashara huyo amepigwa faini ya sh.500,000 kulingana na sheria za TFDA na kwamba ametoa rai kwa wafanyabiashara kuacha kuwauzia wananchi bidhaa ambazo zimeharibika au kumalizika muda wake.“Natoa wito kwa wananchi kabla ya kununua bidhaa yoyote wajiridhishe kwa kusoma tarehe ya kutengenezwa bidhaa na mwisho wa matumizi ili kuepuka kununua bidhaa ambazo zimeharibika zinazoweza kuleta athari kiafya kwa mtumiaji’’,anasisitiza Mkomela.

Mfamasia Wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Ndavitu Sanga anatahadharisha watu wenye ulemavu wa ngozi(Albino) katika Manispaa hiyo kuwepo kwa mafuta feki ya kupaka aina ya Sunblock cream UV40 kwa ajili ya Albino yanayosaidia kujilinda dhidi ya saratani ya ngozi.Kulingana na Sanga mafuta feki ya albino yanauzwa kati ya sh.3500 hadi 6000 na mafuta halisi yanauzwa kati ya sh.40,000 hadi 90,000.

Taarifa imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Manispaa ya Songea

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa