• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TUPINGE UKATILI WA KIJINSIA.

Tarehe ya kuwekwa: December 11th, 2020

Ukatili wa kijinsia ni kitendo ambacho kinafanywa na mtu kwa  kumfanyia mtu mwingine bila kujali umri, maumbile,  kabila,  rangi,  dini, lakini matukio mengi  huwagusa wanawake na watoto kwa  Kwakufanyiwa ukatili wa kimwili, kingono, kiuchumi na kisaikolojia.

Hayo yamebainika siku ya kilele cha maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia na watoto yalifanyika katika viwanja vya zimanimoto tarehe 10 disemba 2020 yaliyodhaminiwa na wadau kutoka USAID- Boresha afya kwa  lengo la  kukuza uelewa juu ya ukatili wa kijinsia kutoka ngazi ya chini ya jamii hadi ngazi ya Taifa.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa  Mkuu wa wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema ambaye aliwakilishwa na Katibu Tawala  Wilaya Pendo Daniel ambaye alianza kwa kutembelea vibanda vya  maonesho mbalimbali ikiwemo na Upimaji wa Virus Vya Ukimwi.

Pendo alisema “ ni lazima tutambue kuwa hiyo ni fursa ya pekee ambayo hutoa nafasi ya kuhamasisha na kuelimisha jamii kuhusu haki za binadamu hususani haki za wanawake na watoto ambao hunyanyasika sana kutokana na unyonge walionao, na hatuna budi kuitumia fursa hiyo kwa ajili ya kuelimisha jamii, na kukemea vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia kama ukandamizaji wa wanawake na watoto”.

Serikali kupitia Wizara ya Afya, maendeleo ya jamii, Wazee na watoto ili kuandaa na kutekeleza Mpango huu wa watoto ( MTAKUWA 2017/2021) ukiwa umejidhatiti   kusimamia mambo yote yanayohusu ulinzi wa mwanamke na mtoto.

Naye Afisa Ustawi wa jamii Manispaa ya Songea Devotha Ndunguru  alisema”  ukatili wa kijinsia unaweza kusababisha Migogoro ya ndoa,  maambukizi ya VVU, ulemavu wa kudumu, upotevu wa maisha, mauaji ya watoto, mimba za utotoni, kuugua,  na mauaji ya watoto wa mtaani.

Ili kuepukana na madhara yatokanayo na ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto ambapo  alisema hatuna budi kuleta  ushirikiano kwa wadau wote wakiwemo wadau wa Afya, polisi, ustawi wa jamii, maendeleo ya jamii, mahakama, pamoja na jamii kwa ujumla ili kutokomeza vitendo vinavyosababisha ukatili wa kijinsia.  “Devotha alibainisha”.

Alisema mwaka 2019/2020 mashauri ya watu waliofanyiwa unyanyasaji wa kijinsia me 439, ke 469 kati ya hizo  kesi zilizopo mahakamani 236, na  zilizoshinda kesi 36.

Amezitaja Sababu ambazo husababisha ukatili wa kijinsia ni pamoja na  uelewa mdogo wa wananchi juu ya ukatili wa  kijinsia, Umaskini, ukosefu wa elimu, ulevi,  wivu wakimapenzi, mapungufu katika sheria pamoja na sababu za kiuchumi.

Alitabanaisha kuwa  wahanga wa ukatili wa kijinsia walio wengi  hawaripoti matukio kwasababu ya mila potofu, uelewa duni, umaskini, na kukosekana kwa vyombo vya kushughulikia  ukatili ngazi ya jamii.

Aidha katika kukabiliana na changamoto hizo, Manispaa ya Songea imejiwekea mikakati ya kudhibiti matukio ya ukatili wa kijinsia kama kuimarisha mfumo  wa utoaji huduma kwa wahanga, kuimarisha kamati za ulinzi wa mwanamke na mtoto, na  kuendelea kutekeleza  mpango wa Taifa wa kutokomeza  ukatili dhidi ya wanawake na watoto ( MTAKUWA).

kauli mbiu;     TUPINGE UKATILI WA KIJINSIA MABADILIKO YANAANZA NA MIMI.

 

IMETAYARISHWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA .

11 disemba 2020.

 

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bil. 22.9 Kujenga Masoko ya Kisasa Manzese A na B, na Kiwanda cha Kuchakata Mazao ya Nafaka Lilambo

    July 06, 2025
  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Tazama zote

Video

Makabidhiano ya Mkataba Soko la Manzese A&B
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa