• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TUWAENZI MASHUJAA WA VITA VYA MAJIMAJI KWA KUHIFADHI UTAMADUNI WETU.

Tarehe ya kuwekwa: February 28th, 2022

 

Na;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI; 

MANISPAA YA SONGEA.

28/2/2022

Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. David Silinde (MB)  amezitaka mamlaka za Serikali za mitaa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii kutumia kumbukumbu na historia za Taifa kama chanzo cha ajira kwa wananchi ili kuchangia katika mapambano dhidi ya umaskini nchini.

Amebainisha hayo katika tamasha la kumbukizi ya miaka 115 ya vita vya Majimaji na utalii wa utamaduni iliyofanyika hapo jana tarehe 27 februari 2022 katika eneo la Makumbusho ya Taifa ya vita vya Majimaji lililopo Mtaa wa Mashujaa ndani ya Manispaa ya Songea, tukio ambalo lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka ndani na nje ya Tanzania.

Silinde alisema kuwa njia bora ya kuwaenzi mashujaa wa vita vya Majimaji ni pamoja na kuhifadhi utamaduni kwa kufanya kazi kwa bidii, kulinda rasilimali za Taifa, kupambana na kuzuia rushwa, ujangili na maatumizi ya madawa ya kulevya kwa kutunza maadili ya mila na desturi za kale kupitia kizazi hadi kizazi. ’Alisisitiza’

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Pololet Kamando Mgema ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Songea amewataka wananchi wa Ruvuma kuiga uzalendo wa mashujaa hao kwa kudumisha Amani, mshikamano na umoja kwa kuzingatia misingi ya utamaduni iliyowekwa na mashujaa wa vita vya Majimaji.

Ametoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano katika zoezi la utoaji Anwani za makazi na postikodi pamoja na sensa kwa lengo la kuisadia Serikali katika upangaji mikakati ya maendeleo kwa wannachi wake.

Naye mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Ezekiel Mwakalukwa alieleza kuwa Tamasha hilo hufanyika kila mwaka kuanzia tarehe 25 hadi 27 februari kwa lengo la kuwakumbuka mashujaa waliopigana vita vya Majimaji ambapo mashujaa 67 walinyongwa na wakoloni wa Ujerumani mnamo Februari 27 mwaka 1906 na kuzikwa katika makubiri yaliyopo ndani ya makumbusho ya Taifa ya vita vya Majimaji,  pamoja na kuinua utalii wa utamaduni nchini Tanzania.

Ametoa rai kwa wadau na wanachi wote kwa ujumla kuendeleza uzalendo  pamoja na kuona fursa na kiuchumi zilizopo kupitia utalii wa utamaduni.

Kauli mbiu katika Tamasha hilo ni “Utamaduni wetu, nguvu yetu kwa maendeleo ya Utalii wa uchumi”.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa