• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UCHOMAJI misitu hovyo unavyoiweka Dunia njia panda

Tarehe ya kuwekwa: June 2nd, 2018

TUKIWA katika wiki ya mazingira duniani,uchomaji moto hovyo misitu ya hifadhi na maeneo yaliohifadhiwa kisheria umekuwa  unaleta athari za kimazingira katika maeneo mbalimbali nchini.

Kila mwaka majira ya kiangazi kuna kesi nyingi za uchomaji moto hovyo misitu na mapori ambao unasababisha hasara kubwa kiuchumi lakini pia kuathiri viumbehai wanaoishi katika maeneo hayo.

Kwa mfano mara kadhaa msitu wa serikali wa SAO HILL wenye urefu wa kilometa 60 uliopo Mafinga wilayani Mufindi mkoani Iringa kumekuwa na matukio ya kuchomwa moto.

Msitu huo unapoteketezwa na moto unaleta athari kubwa kimazingira kwa kuwa SAO HILL ni miongoni mwa chanzo cha mto Ruaha mkuu ambao ni muhimu sana kwa viumbehai na uchumi wa Tanzania.

Wataalam wa mazingira wanaonya kuwa msitu wa SAO HILL ukiteketea wote kwa moto unaweza kusababisha hasara kubwa kwa serikali kwa kuwa gharama kubwa ilitumika na serikali kuanzisha msitu huo katika kipindi cha awamu ya kwanza cha hayati Baba wa Taifa mwalimu Julius Nyerere  kwa kuwa serikali ilikopa Benki ya Dunia miaka ya 60 mamilioni ya dola za kimarekani  kwa ajili ya kuanzisha msitu huo.

 

Uchunguzi unaonesha kuwa  msitu wa SAO HILL ni moja ya mapafu ya Tanzania kwa kuwa iwapo itakauka kwa kuchomwa  inaweza kusababisha chanzo cha maji cha mto Ruaha kilichopo katika msitu huo kuathirika hivyo Tanzania inaweza kugeuka jangwa.

Ukiachia msitu wa SAO HILL,Uchomaji moto hovyo pia umekuwa unatokea katika msitu wa serikali wa Matogoro uliopo Manispaa ya Songea na pori la akiba la wanyama la Liparamba wilayani Mbinga  na kuathiri pori hilo ambalo lipo mpakani na nchi  yetu na nchi ya Msumbiji.

Kulingana na uchunguzi,mikoa yote  nchini yenye misitu aina ya miyombo, ina matukio mengi ya moto. Mikoa hiyo ni Rukwa, Mbeya, Tabora, Kigoma, Ruvuma, Lindi, Mtwara, Morogoro  na Pwani.

Uchunguzi pia umebaini kuwa Kutokana na moto kuvuka mipaka ya mikoa bila kujali ulianzia wapi ni vigumu kubaini mkoa gani unaongoza kwa uchomaji moto katika Tanzania.


Hata hivyo ripoti ya Wizara ya Mazingira inataja utekelezaji wa Mkakati wa Kuhifadhi Mazingira ya Ardhi na Vyanzo vya Maji, ambapo Halmashauri za Wilaya, Miji na Majiji, kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii,inaendeleza mikakati ambayo inalenga kudhibiti uchomaji moto.


Sera ya Taifa ya misitu inaelekeza wananchi  kuhifadhi na kuendeleza misitu kwa njia ya usimamizi shirikishi wa misitu.

Sheria ya usimamizi wa mazingira namba 20 ya mwaka 2004 fungu namba 187 kwa makosa yanayohusu uchafuzi wa mazingira ya maji, hewa, ardhi na uchomaji misitu hovyo inaagiza  kuwa mtu yeyote atakayekiuka chochote cha sheria hiyo akitiwa hatiani atatozwa faini isiyozidi milioni 50 au kifungo kisichozidi miaka saba jela ama vyote viwili.

Wiki ya mazingira duniani huadhimishwa kila mwaka kuanzia Mei 31 na kilele chake Juni 5,ambapo mwaka huu katika mkoa wa Ruvuma maadhimisho hayo yanafanyika Kata ya Mjimwema Manispaa ya Songea,mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme.

 

Makala hii imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Juni 2,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa