Mkurugenzi wa Usimamizi wa Elimu kutoka ofisi ya Rais TAMISEMI Vicent Kayombo amewataka wataalam kusimamia miradi kwa weredi ili iweze kujengwa kwa ubora na viwango vinavyotakiwa.
Alisema Serikali imeweka utaratibu wa kutoa mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu ngazi ya Halmashauri na Mkoa kwa lengo la kuimarisha usimamizi wa miradi ya Serikali ili kufanikisha lengo tarajiwa.
Hayo yamejili katika mafunzo ya wataalamu zaidi ya 280 kutoka Mkoa wa Iringa, Njombe, na Ruvuma yaliyotolewa na Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu , Sayansi na Teknolojia kupitia mradi wa BOOST yaliyofanyika kuanzia tarehe 16-17/2022 katika kanda 9 katika Mkoa wa Iringa.
Akizungumza na washiriki wa mafunzo elekezi kwa timu za utekelezaji wa mradi wa BOOST kutoka kwenye Halmashauri na Mikoa alisema lengo kuu mahususi la mafunzo haya ni pamoja na kuzijengea uelewa timu za utekelezaji kuhusu mradi wa BOOST ambao utazingatia usimamizi wa fedha na manunuzi ya umma, kuandaa mpango wa utekelezaji wa boost, afua zitakazotekelezwa kupitia mradi wa boost.
Mradi huo wenye thamani ya takribani Trioni 1.15 sawa na Dola za kimarekani Milion 500 ambapo kati ya hizo Dola za Kimarekani 480, ni programu na Dola za Kimarekani Milioni 20 ni gharama ya uwekezaji wa mradi.
Mradi huo utafanyika kwa muda wa miaka 5 kuanzia 2021/2022 hadi 2025/26 ambapo utatekelezwa kwa awamu tofauti ambayo itajengwa madarasa 12,000 ya awali na shule za msingi 3000 kwa mwaka, kununua vifaa vya TEHAMA kwa shule zaidi ya 800 za msingi na vituo vya walimu kwa ajili ya kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji na mafunzo endelevu ya walimu kazini.
Mradi huo utasaidia kuongezeka kwa uandikishaji wa Elimu ya awali kutoka asilimia 76.9% kwa mwaka 2021 hadi asilimia 85% pamoja na kutekeleza mafunzo ya walimu kazini (MEWAKA) katika ngazi ya vituo vya walimu.
Miongoni mwa washiriki katika mafunzo hayo ni Afisa elimu kutoka kila Halmashauri na Mkoa, Afisa manunuzi, Afisa mipango, Afisa maendeleo ya jamii, Mhandisi, Mdhibiti ubora, Mratibu wa mradi, Katibu wa TSC Wilaya, Mhasibu, Mwalimu mkuu kutoka kila Halmshauri, na Afisa Habari kutoka ngazi ya Mkoa na Halmashauri.
Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya jamii TAMISEMI Hilda Mgomapayo alisema utekelezaji wa afua hiyo ni mpango salama kwa Elimu ya awali na msingi ambao unalenga kupunguza vikwazo vya upatikanaji wa elimu kwa watoto wote na waliopo katika mazingira hatarishi wakiwemo na wenye mahitaji maalumu pamoja na kuwezesha kukamilika mzunguko wa Elimu.
Mgomapayo alisema katika kipindi cha miaka mitano ya kwanza mpango wa shule salama unalenga kuzifikia shule 6000 hadi kufikia 2026 kwa lengo mahususi la kuweka mazingira ya mapito salama kwa wanafunzi wanapokwenda shule na kurudi nyumbani. “alibainisha”
IMEANDALIWA NA;
AMINA PILLY;
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.
SONGEA MUNICIPAL COUNCIL
Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA
Simu ya Mezani: 025 2602970
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@songeamc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa