• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UGAWAJI WA DAWA ZA KICHOCHO SHULENI KWA WANAFUNZI WENYE UMRI WA MIAKA 5 - 14 MANISPAA YA SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: September 17th, 2020

Afisa wa Mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele  Frank Komakoma alisema lengo la serikali ni kuhakikisha zoezi hili la ugawaji wa dawa linatekelezwa vizuri ili kila mtoto/mwanafunzi aweze kupewa dawa hizo.

Komakoma alitamka hayo akiwa katika mafunzo kwa walimu wakuu wa shule za msingi 91, waratibu elimu kata 21, walimu wa afya, na  wataalamu  Sekta ya elimu kwa ajili ya kuwaandaa katika kusimamia zoezi la ugawaji wa dawa za minyoo ya tumbo na kichocho  kwa wanafunzi 58,000 wenye umri wa miaka 5-14 linalotarajia kufanyika kuanzia  18.09 hadi 21.09.2020  Manispaa ya Songea.

Alisema Wizara ya Afya imeweka malengo mkakati ya utekelezaji  wa mpango wa kuongeza upatikanaji wa huduma, tiba na kujenga uwezo wa utekelezaji wa mpango huu kwa jamii ili jamii iwe na afya bora.

Naye Mratibu wa kanda ya Chabruma Manispaa ya Songea dr. Stephen Chacha alisema “ magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ni magonjwa ambayo yamo ndani ya jamii maskini lakini jamii yenyewe na hata wataalam husika ama viongozi hawayapi umuhimu kulingana na madhara yake katika jamii. Akiyataja magonjwa hayo ni usubi, Matende na mabusha, Trakoma, kichocho na  minyoo ya tumbo.”

Dr. Chacha alisema kichocho husababishwa na minyoo inyoitwa jamii ya Schistosoma ambao unaenezwa na konokono kwa kutoa vimelea kupitia maji yaliyotuama.

Alisema kichocho husababisha damu kutoka kwenye njia ya mkojo na choo, na baadae inaweza kusababisha saratani ya tumbo, kibofu cha mkojo na ini.

Aliongeza kuwa minyoo ya tumbo imegawanyika katika aina tatu 3 nayo ni minyoo mviringo, minyoo mjeledi, na minyoo ya safura ambayo huishi kwenye udongo na husababisha mtu kuwa dhaifu na kuishiwa damu na isipotibiwa mapema inaweza kusababisha utumbo kujifunga na kifafa, pia inaweza kumfanya mtoto ashindwe kuhudhuria shule au kutoelewa vizuri.

Alizitaja njia za kujikinga  na magonjwa hayo ni pamoja na kutumia dawa za kutibu na kudhibiti magonjwa haya ambazo hutolewa kila mwaka kwa jamii iliyoathirika, kuzingatia usafi wa uso na mwili, usafi wa mazingira, kutokuoga kwenye maji yasiyo safi na yaliyotuama (bwawa), kujikinga kuumwa na inzi au  mbu, na  kutoa elimu ya afya ya jamii.

Alisema kwa ugonjwa wa kichocho unatakiwa kumeza dawa ya praziquantel kwa miaka mitano mfululizo, ugonjwa wa minyoo ya tumbo  na usubi na matende  hutumika katika kujikinga na kutibu kwa dawa ya Mectizan na Albendazole, ugonjwa wa trakoma hutumia kutibu dawa ya Zithromax.

Aidha,  imefafanuliwa kuwa mwalimu amepewa moja ya majukumu  ya kutoa elimu ya afya kuhusu manufaa na maelekezo ya umezaji dawa husika kwa kiongozi wa shule, wazazi, na wanafunzi, kuandikishwa walengwa (wanafunzi) kwenye rejista, kuaandaa chakula kwa ajili ya wanafunzi kabla ya kumeza dawa na Dawa hiyo imezwe ndani ya masaa mawili baada ya kula chakula.  

Naye afisa elimu Manispaa ya Songea Zakia Fandey amesema atahakikisha anasimamia vizuri shule zote na atahakikisha kila mtoto aliyeandikishwa shule anapewa dawa hizo.

IMETAYARISHWA NA;

AMINA Y. PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

17.09.2020

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa