• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UKWELI kuhusu miti ya mikaratusi kudaiwa kunyonya kiwango kikubwa cha maji

Tarehe ya kuwekwa: December 29th, 2018

TAFORI kuhusu ukweli  wa miti ya kigeni na matumizi ya maji imebainisha kuwa  mwaka 2000 eneo la mashamba ya miti ya kigeni aina ya mikaratusi duniani kote lilikaribia hekta milioni 18 kati ya hizo asilimia 37 ya eneo hilo lilikuwa barani Afrika na asilimia 73 ya eneo hilo lipo Afrika ya kusini. MITI aina ya mikaratusi inadaiwa inaongoza kwa kunyonya kiwango kikubwa cha maji ardhini hali ambayo inachangia kuharibu vyanzo vya maji pale inapopandwa jirani na vyanzo hivyo.

Kuna taarifa kuwa mti mmoja mkubwa wa mkaratusi una uwezo wa kunyonya maji kiasi cha milimita 300  kwa siku kutoka ardhini hivyo katika maeneo mengi vyanzo vya maji ambayo imepandwa miti hiyo inadaiwa imeua vyanzo vya maji na kusababisha ukame.

Kwa mfano katika msitu wa serikali uliopo milima ya Matogoro nje kidogo ya mji wa Songea ,imepandwa miti aina ya mikaratusi ambayo inatajwa kuchangia kuharibu vyanzo vya maji vilivyopo katika milima hiyo ambavyo ni muhimu kwa kuwa vinatumika kusambaza maji yanayotumiwa na Mamlaka ya Maji Safi na Taka Songea SOUWASA kusambaza maji katika manispaa ya Songea.

Pia katika msitu wa mlima Matogoro kuna chanzo cha mto Ruvuma ambao ni maarufu kwa kuwa ni miongoni mwa mito mikubwa Tanzania ambao unamwaga maji yake Bahari ya Hindi.Mto huo pia unatenganisha nchi ya Tanzania na Msumbiji.

Kutokana na hali hiyo  serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii iliamuru miti yote aina ya mikaratusi katika msitu wa serikali wa Matogoro kuvunwa kwa wakati mmoja  ili kuepuka ukame na kupanda miti ya asili inayokua polepole ambayo ni rafiki katika vyanzo vya maji.

Hata hivyo Utafiti wa kisayansi unaonesha kuwa sio miti yote aina ya mikaratusi ikiwemo ya milima ya Matogoro ina tabia ya kunyonya maji kwenye vyanzo vya maji.

Utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Misitu nchini (TAFORI) unaonesha kuwa kuna aina ya miti ya mikaratusi ambayo ni rafiki wa vyanzo vya maji ndiyo maana katika misitu mingine nchini kama ile ya Sao Hill Mafinga Mkoa wa Iringa imepandwa miti ya mikaratusi tena karibu na vyanzo vya maji ambavyo vimeendelea kutoa maji na hakuna dalili zozote za ukame au maji kupungua.

TAFORI pia imebaini kuwepo kwa aina kadhaa ya miti  aina ya mikaratusi ambayo kwa kiwango kikubwa inanyonya maji mengi.

Kulingana na utafiti wa TAFORI miti hiyo ni Mikaratusi jamii ya Camaldulensis ambayo hunyonya maji kiasi cha milimita 1,240 kwa mwaka na Mikaratusi aina ya Microrhea inayonyonya maji milimita 1,050 kwa mwaka, Mikaratusi ya aina ya Patula nayo hunyonya maji kiasi cha milimita 665 kwa mwaka.

 

Changamoto iliyopo hivi sasa ni kwamba miti mingi aina ya mikaratusi imekwishaondolewa  isipokuwa tatizo la kujiotea kila inapovunwa ndilo linalosumbua na kuathiri miti ya asili ambayo imepandwa.

Taarifa ya TAFORI  inabainisha kuwa mashamba mengine  makubwa ya mikaratusi barani Afrika yapo katika nchi za Morocco,Angola,Ethiopia na Tunisia  na kwamba katika Afrika mashariki nchi ya Kenya inaongoza  kwa mikaratusi ikifuatiwa na Uganda na Tanzania na kwamba maeneo ya mikaratusi katika nchi za Burundi na Rwanda ni maradufu ya maeneo ya nchi ya Kenya.

Kutokana na utafiti huo TAFORI inabainisha kuwa Tanzania haijumuishi kwenye nchi maarufu kwa upandaji wa mikaratusi na kwamba haiwezi kuchukua nafasi ya kwanza kubaini madhara ya mikaratusi.

Hata hivyo utafiti ambao umetolewa  na TAFORI kuhusu   miti ya kigeni na matumizi ya maji unaonesha kuwa  mikaratusi  iliyopo katika nchi ya Sudan kwa mwaka matumizi yake ya maji ni milimita 1240 wakati mikaratusi katika nchi ya Pakstani matumizi ya maji kwa mwaka ni milimita 1500.

Utafiti huo unaonesha kuwa mikaratusi iliyopo nchini Kenya kwa mwaka matumizi ya maji ni milimita 830 na miti aina ya misindano Tanzania katika msitu wa Sao hill Mafinga  kwa mwaka hutumia maji milimita 665.

Kulingana na utafiti huo matumizi ya maji kwa mwaka kwa miti mingine na mazao ukilinganisha na mikaratusi unaonesha kuwa miti aina ya mvinje iliyopandwa  Bura nchini Kenya  kwa mwaka inatumia maji  milimita 5437, jamii ya mpingo katika eneo la Bura Kenya kwa mwaka inatumia maji milimita 1143 na Mgunga nchini Paktan unatumia milimita 2100 za maji kwa mwaka.

Utafiti huo unaonesha kuwa mazao ya kilimo nchini Pakstani yakiwemo ngano kwa mwaka yanatumia milimita 330 za maji,pamba milimita 460,mahindi nchini Marekani kwa mwaka yanatumia maji milimita 630 na pamba ya Marekani inatumia maji milimita 630.

Zao la korosho hapa nchini katika Wilaya ya Nachingwea kwa mwaka linatumia maji milimita kati ya 814 hadi 1409,mpunga nchini Pakstan kwa mwaka unatumia maji milimita  1620 na miwa katika nchi ya Pakstani inatumia maji milimita 1400 kwa mwaka.

Utafiti huo unaonesha kuna miti kama mvinje na mgunga inatumia maji mengi kuliko mkaratusi na kwamba yapo baadhi ya mazao kama mpunga na miwa ambayo yanatumia maji karibu sawa au zaidi ya mikaratusi.

 

Miaka ya karibuni Wizara ya Maliasili na Utalii,  baadhi ya viongozi,na wadau wa mazingira wameilaumu mikaratusi(eucalyptus) iliyopandwa katika Msitu wa Serikali Matogoro Wilaya ya Songea kutokana na kudaiwa miti hiyo inanyonya maji katika kiwango kikubwa na kutishia vyanzo vya maji vilivyopo katika msitu huo.

Kutokana na hali hiyo yalifanyika maazimio ya kuing’oa miti hiyo  kwenye msitu wa serikali wa milima ya Matogoro na kupanda miti ya asili .

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa