• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UMEME wa Grid kuwashwa Songea Septemba

Tarehe ya kuwekwa: June 25th, 2018

MKUU wa Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma,Pololet Mgema amekagua  Ujenzi wa Kituo cha kupooza Umeme kilichopo Unangwa Manispaa ya Songea na kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa kituo hicho

Mgema amesema serikali imedhamiria kuhakikisha Mkoa wa Ruvuma unaunganishwa na umeme wa Grid ya Taifa kutokea Makambako hadi mjini Songea kupitia Madaba.

Juni 24 mwaka huu TANESCO ilizima njia ya kusafirishia umeme  ya 220k Mufindi-Mbeya ili kuruhusu mafundi kuingiza umeme katika kituo kipya cha Madaba mkoani Ruvuma.

Kituo cha kupoozea Umeme cha Unangwa mjini Songea ni moja kati ya vituo vitatu vya kupooza umeme wa msongo mkubwa wa 220kv kabla ya kuupeleka kwa watumiaji.

Vituo vingine vya kupoozea umeme ni  Madaba Wilayani Songea na Makambako Mkoani Njombe.

Taarifa ya Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO) inaonesha kuwa njia kuu ya kusafirisha Umeme wa Msongo Mkubwa kutoka Makambako umekamilika kwa asilimia kubwa na kwamba kazi zilizobaki ni ukamilishaji wa vituo hivyo vya kupoozea umeme.

Kulingana na TANESCO umeme wa Grid ya Taifa unatarajiwa kuwashwa mjini Songea Septemba mwaka huu na kazi ya kusambazwa kwa watumiaji inaendelea kufanywa na Shirika hilo.

Tangu mwaka 2016 tatizo la mgawo wa umeme katika mji wa Songea limebakia kuwa historia mara baada ya TANESCO Ruvuma kuanza kununua umeme wa maji kutoka Tulila mto Ruvuma.

Chanzo hicho cha maji kinamilikiwa na Watawa Wabenediktine wa Mtakatifu Agnes Chipole Jimbo Kuu Katoliki la Songea ambapo hadi sasa wana mashine mbili zenye uwezo wa kuzalisha megawati tano,lengo ni kuzalisha umeme megawati 7.5.

Mahitaji ya umeme katika mji wa Songea ni kilowatts 4300 hivyo basi kutokana na umeme wa maji unaozalishwa Tulila,TANESCO Ruvuma imefanikiwa kumaliza kabisa tatizo la mgawo wa umeme katika mji wa Songea.

TANESCO Ruvuma hivi sasa inatumia umeme wa Tulila katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea,Halmashauri ya Wilaya ya Songea,Mbinga na Nyasa.

Baada ya kukamilika kwa mradi huu mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia mafuta mazito hapa Songea, Madaba na Mbinga itazimwa na kupelekea kuokoa gharama kubwa zinazotumika na TANESCO kuzalisha umeme.

Mkuu wa Wilaya ya Songea anawakaribisha Wawekezaji Wazawa na Wageni kuwekeza katika wilaya hiyo Songea kuwekeza katika ujenzi wa viwanda kwa sababu sasa wilaya ya Songea itakuwa na umeme wa kutosha,uhakika na kuaminika.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Juni 25,2018

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa