• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UMEME wa Grid ya Taifa wawashwa kwa mara ya kwanza mkoani Ruvuma

Tarehe ya kuwekwa: September 14th, 2018

HATIMAYE umeme wa Gridi ya Taifa umefika mjini Songea na Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla  kupitia Makambako na Madaba. Mashine za Mafuta (Diesel Generetors) za Madaba zimezimwa rasmi na wananchi wanafurahia umeme wa Gridi.Tayari Wizara ya Nishati kupitia TANESCO imewaangazia maisha Wananchi wa mkoa wa Ruvuma.

Hata hivyo Waziri wa Nishati Dkt.Merdad Kaleman amesema Ifikapo Septemba 26 mwaka huu itawashwa mitambo yote na wananchi wataanza rasmi kutumia umeme kutoka kwenye mradi huu wa Makambako-Songea“Tukiwasha mitambo ya mradi huu tutazima rasmi mitambo ya umeme iliyokuwa inatumia mafuta mazito iliyoko Madaba, Ludewa, Mbinga, Namtumbo na Songea Mjini’’,anasisitiza Waziri wa Nishati.

Serikali imejenga mradi mkubwa wa kusafirisha umeme wa Grid ya Taifa kutoka Makambako mkoani Njombe,kupitia Madaba hadi Songea mjini umbali wa kilometa 250 ili umeme wa kutosha uweze kuwafikia wananchi na utumike kwa maendeleo endelevu.

Serikali imejenga vituo vya kupoozea umeme huo wa Grid ya Taifa na kuuongeza nguvu kutoka kilovolti 132 hadi kilovolti 220 ambao utakuwa umeme mkubwa kwa matumizi ya viwanda.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa umeme wa REA mkoani Ruvuma,Waziri wa Nishati Dkt.Merdad Kalemani aliahidi kuwa umeme wa Grid ya Taifa utawashwa mjini Songea Septemba 2018 jambalo liliahidiwa na limetekelezwa kwa wakati.

Waziri Dkt.Kalemani alisisitiza kuwa  umeme huo wa Grid ya Taifa pia utatumika kusambaza umeme katika vijiji  120 vya mkoa wa Ruvuma na Njombe na kwamba umeme huo utatoa umeme kwa wateja wapya 22,700.

Kulingana na Waziri Kalemani, umeme huo utasambazwa katika wilaya zote za mkoa wa Ruvuma na wilaya za Ludewa na Njombe mkoani Njombe umbali wa kilometa 900 hivyo kuwezesha sasa mkoa wa Ruvuma kuanza kupata umeme wa uhakika na kuaminika hivyo kufungua fursa za uchumi wa viwanda.

Waziri Kalemani anawashauri watanzania kutumia umeme kwa kujenga viwanda vidogo na kusindika mazao mbalimbali ambayo yanalimwa katika mkoa wa Ruvuma yakiwemo Mahindi, Kahawa,korosho,alizeti na mazao ya matunda ili kuongeza thamani ya mazao wanayozalisha.

Sera ya Serikali ni kuhakikisha kuwa wananchi wengi wanapata nishati ya umeme,ambapo takwimu zinaonesha kuwa idadi ya watu wanaopata nishati ya umeme nchini imepanda toka asilimia 10 mwaka 2010 hadi kufikia asilimia 67 mwaka 2017.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari serikalini 

Septemba 14,2018


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa