• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UTAFITI:TABIA ya Sokwe inafanana na binadamu kwa asilimia 98

Tarehe ya kuwekwa: May 18th, 2018

UTAFITI umeonesha kuwa, asilimia zaidi ya 96 ya chembe za urithi za binadamu zinafanana na zile za sokwe, pia ubongo wa sokwe na vitendo  vyao vinafanana sana na vile vya binadamu.

Profesa Richard  wa somo la viumbe kutoka Chuo Kikuu cha Harvard nchini Marekani anaeleza kuwa, sokwe ni daraja pekee kati ya binadamu na maumbile hivyo ni vema wanyama hao kulindwa kwa nguvu zote.

Mhifadhi wa Hifadhi za Taifa,Noelia Mnyonga  anasisitiza tafiti za kisayansi zimethibitisha kuwa Sokwe ni wanyama ambao wanafanana  na binadamu katika tabia kwa asilimia 98  na kusisitiza kuwa ndiyo maana wanaitwa sokwe mtu.

“Sokwemtu ni mnyama ambaye alibakiza asilimia mbili tu angeweza kufanana na binadamu kitabia kwa asilimia 100 hali ambayo inamfanya mnyama huyu kutafutwa kwa udi na uvumba baada ya kuwa kivutio adimu na cha kipekee cha utalii duniani kote’’,anasema Mnyonga.

Mnyonga anasisitiza kuwa sokwe mtu ni mnyama wa ajabu ambaye kwa tabia na matendo hatofautiani sana na binadamu  ndiyo maana baadhi ya watu wanamuita binadamu pori.

Sokwe mtu ni mnyama ambaye ni mfano halisi wa binadamu, mnyama huyu anavutia macho ya watalii wengi,ambao wanamiminika hapa nchini katika hifadhi ya Taifa ya Gombe kwenda kuwashangaa wanyama hao adimu na wa aina yake.

Tafiti za kisanyansi zinaonesha kuwa sehemu ya ubongo  wa sokwe  inafanana na sehemu ya ubongo wa binadamu,hali hiyo ndiyo imesababisha sokwemtu kufanya matendo mengi ambayo yanafanywa na binadamu kwa mfano sokwemtu anaweza kupiga mswaki,kula chakula na kucheza kama binadamu.

“Sokwe anaweza kufanya mambo mengi kama anavyofanya binadamu, hali hiyo imewavutia watalii na watafiti wa kimataifa kufika katika hifadhi ya Taifa ya Gombe kufanya uchunguzi wa kina kuhusu  tabia za wanyama hawa”,anasema mhifadhi Mnyonga.

Hifadhi ya Taifa ya Gombe ilipata umaarufu duniani baada ya mtafiti wa tabia za sokwe duniani Dk.Jane Gooddall raia wa  nchi ya Uingereza kufanya utafiti kuhusu maisha na tabia ya sokwe wa Gombe kwa muda wa miaka 40 na kuandika vitabu kadhaa kuhusu wanyama hao.

Dk.Goodall ndiye alitoa tahadhari  ya  kuhakikisha kuwa wanyama hao walio na ukoo wa karibu na mwanadamu hawaangamii kabisa na kuonya iwapo hatua za makusudi hazitachukuliwa  za kuwalinda, sokwe wanaweza kuangamia.

Mwanasayansi Dk.Gooddall anasema katika nusu karne iliyopita, idadi ya sokwe ilipungua kutoka takribani milioni mbili hadi kufikia laki tatu pekee katika nchi 21, ambapo hivi sasa hali ni mbaya zaidi kutokana na aina adimu ya sokwe wamesalia Tanzania pekee.

Tanzania ina Hifadhi za Taifa 16 ambazo ni hifadhi ya Taifa Arusha,Gombe,Katavi,mlima Kilimanjaro, Mahale, Mikumi, Ziwa Manyara,Ruaha,Rubondo, Serengeti, Saadan, Tarangire, Udzungwa,Kitulo, Mkomazi na Saanane.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Mei 18,2018

 

 

                     

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa