• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

VIJANA 153 kupewa mafunzo ya ujasiriamali na biashara mkoani Ruvuma

Tarehe ya kuwekwa: August 11th, 2019

VIJANA  153 katika Mkoa wa Ruvuma wanatarajia kupata mafunzo ya ujasiriamali na biashara kwa viajana  yanayotolewa na Baraza la Taifa la uwezeshaji wananchi kiuchumi (NEEC).

Akitoa taarifa katika ufunguzi wa mafunzo awali  ya ujasiriamali kwa vijana 50 kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea, Mwakilishi wa NEEC Silas Daudi alisema katika mafunzo hayo jumla ya vijana 153 wanatarajia kupata mafunzo hayo ili waweze kushiriki kikamilifu katika ujenzi Taifa.

Alisema mafunzo hayo ni sehemu ya program ya Ujasiriamali kwa vijana wenye umri kati ya miaka 18 -35 katika mikoa ya Tanzania Bara yenye lengo la kuwezesha na kuboresha mbinu za uendeshaji na usimamizi wa biashara na urasimishaji wa shughuli za uzalishaji mali zinazofanywa na vijana.

Daudi aliyataja malengo mengine ya mafunzo hayo kuwa ni kuwawezesha vijana wanaomiliki biashara katika mkoa husika kukuza na kurasimisha biashara zao ili kuongeza ajira kwa vijana wenzao na kuchangia kikamilifu katika pato la taifa.

Kwa mujibu wa Mwakilishi na NEEC, mafunzo hayo yatafanyika katika mikoa nane,ukiwemo Mkoa wa Dodoma ambako mafunzo yameshafanyika kwa vijana 204 na kwamba katika Mkoa wa Ruvuma ambako mafunzo yanafanyika sasa.

 Ameitaja mikoa mingine ambayo mafunzo hayo yatafanyika kuwa   ni Geita, Mwanza, Lindi, Mbeya, Tanga na Arusha.

Mgeni rasmi katika ufunguzi wa mafunzo hayo Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ( NEEC) Beng’i Issa alisema NEEC inasimamia programu ya mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana kujiajiri ambayo hivi sasa inatekelezwa katika mikoa mitano.Lengo likuwa  ni kuchukua vijana ambao hawajasoma na wanaotoka katika familia masikini.

“Kupitia program hii vijana wanapata mafunzo kwa vitendo,wanafuatiliwa,na wanapewa wafanyabiashara wenye uzoefu kuwatembelea kwa muda wa mwaka mmoja.” alisisitiza Issa.

Katibu Mtendaji huyo alisema wametoa muongozo wa kufundisha somo la ujasiriamali katika shule za msingi, sekondari hadi vyuo vikuu.

Naye mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa Ruvuma Hakimu Mafuru ameiomba serikali kutunga vitabu ambavyo vinaelezea mada za  ujasiriamali ili kuwajengea uwezo vijana.

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Phillip Benno, alisema Halmashauri imejipanga kuwa kutumia asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kuwawezesha vijana.

Programu ya mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana  inatarajia kuwanufaisha vijana 40,000 katika mikoa yote ya Tanzania Bara.

Imeandikwa na Farida Mussa

Wa Kitengo cha TEHAMA Manispaa ya Songea

Agosti 10,2019

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa