• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

VIJANA 55 wahitimu mafunzo ya Askari wanyamapori Namtumbo

Tarehe ya kuwekwa: June 24th, 2018

JUMLA ya vijana 55 wamehitimu kozi ya miezi mitatu ya Askari wanyamapori vijijini(VGS) katika chuo cha Uhifadhi wa Maliasili kwa Jamii(CBCTC) kilichopo Likuyu Sekamaganga wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma.

Mgeni rasmi katika mahafali hayo  namba 63 ya mwaka 2018 alikuwa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Generali Gaudence Milanzi.Akizungumza katika mahafali hayo Katibu Mkuu huyo amewapongeza wahitimu wote kufanikiwa kumaliza mafunzo hayo ambayo ni muhimu kwa uhifadhi wa maliasili katika maeneo ya vijijini ambako kuna rasimali nyingi za nchi zinazotakiwa kulindwa.

Ujangili hususani wa tembo umekuwa ni changamoto na tishio kwa nchi yetu na ustawi wa rasilimali hizo,licha ya serikali kujitahidi kufanya kila linalowezekana ili kukomesha ujangili huo kwa kweli ujangili wa tembo bado upo,tunataka kufikia sehemu ambayo tunaweza kusema hatuna ujangili Tanzania’’,alisisitiza Milanzi.

Hata hivyo amesema pamoja na mafanikio ambayo serikali imeyapata katika mapambano dhidi ya ujangili,bado ujangili upo sio kwa tembo tu bali hata wanyama wengine wanauawa kwa sumu ambapo Wizara ya Maliasili imepoteza simba katika baadhi ya maeneo kwa kuwa sumu.

Awali akitoa taarifa ya chuo cha Mafunzo ya Uhifadhi wa Maliasili Kwa Jamii (CBCTC) ,Mkuu wa chuo hicho Jane Nyau  alisema wanachuo 55 ambao wamehitimu Juni 24,2018,walianza mafunzo Machi 23,2018 wakiwa jumla ya washiriki 56 kati yao wanaume 38 na wanawake 18.

“Washiriki 50 wanafadhiliwa na Shirika la WWF na sita wanafadhiliwa na Shirika la Carbon Tanzania lililoko mkoani Arusha,hata hivyo washiriki 55 ndiyo wametunukiwa vyeti mshiriki mmoja aliahirisha kozi kutokana na matatizo ya kiafya’’,alisisitiza.

Chuo cha CBCTC kilianzishwa mwaka 1995 na Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii,lengo likiwa ni  kutekeleza sera ya wanyamapori inayosisitiza ushirikishwaji wa jamii katika uhifadhi wa rasilimali za maliasili.

Kwa mujibu wa Mkuu wa CBCTC,chuo hicho kimefanikiwa kuijengea jamii uwezo kwa njia ya mafunzo ili kuiwezesha kushiriki kikamilifu katika uhifadhi na matumizi endelevu ya maliasili ambapo tangu kuanzishwa kwake hadi sasa jumla ya wananchi 4512 wamepata mafunzo kati yao wanaume 3804 na wanawake 708.

Mwandishi ni Albano Midelo

Mawasiliano albano.midelo@gmail.com,simu 0784765917

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Chupa 14,789 za Damu Kukusanywa Mkoani Ruvuma

    June 04, 2025
  • Mazishi ya Muasisi wa TANU Alhaji Mustapha Songambele

    June 03, 2025
  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • Tazama zote

Video

katibu Mkuu CCM Taifa Aongoza Maziko ya Alhaji Songambele
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa