• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

VITA ya kiuchumi katika sekta ya madini

Tarehe ya kuwekwa: June 13th, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.John Magufuli tayari ametangaza kuwa tupo katika vita ngumu ya kiuchumi katika sekta ya madini, ni vita kubwa na hatari zaidi duniani kwa kuwa inayahusu mataifa makubwa yenye uwezo kiuchumi.

Hii ni vita kubwa kwa kuwa Kampuni za uwekezaji katika sekta ya madini zinatoka mataifa ya magharibi yanatumia mbinu mbalimbali kuhakikisha kuwa nchi za Afrika ambazo zina utajiri wa madini zinaendelea kupoteza huku mataifa hayo yakiendelea kuneema na rasilimali za Afrika.

Katika kutekeleza agizo la Rais la kukabiliana na vita ya kiuchumi katika sekta ya madini,Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa amefanya ziara kwenye mgodi wa dhahabu wa Buzwagi uliopo wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga na kuchukua sampuli za mchanga katika makontena kwa lengo la kwenda kuyapima kwa wataalamu wa madini ili kubaini kiasi cha dhahabu kilichomo.

Hata hivyo uchunguzi umebaini kuwa kuna sababu mbalimbali ambazo zinasababisha Tanzania na nchi mbalimbali za Afrika kuendelea kupoteza katika sekta ya madini.

Rais Magufuli aliteua Kamati maalum ya wajumbe wanane kuchunguza aina na viwango vya madini yaliyomo kwenye mchanga wa madini uliomo ndani ya makontena yaliyozuiliwa na Serikali kusafirishwa nje ya nchi.Uteuzi wa kamati hiyo ulifanywa Machi,29,2017. Wajumbe wa Kamati hiyo ni  wana taaluma katika fani za jiolojia, kemia, uhandisi kemikali na uhandisi uchenjuaji madini.

Chimbuko la kufanyika kwa uchunguzi huu ni kutokana na ukweli kuwa viwango vya madini yaliyopo kwenye makinikia havijulikani, na hata mikataba ya uchenjuaji makinikia haipo wazi.Hali hii inaleta hisia kuwa nchi inaibiwa na hainufaiki na uchimbaji wa madini.

Katika kutekeleza uchunguzi huu,Kamati iliongozwa na Hadidu za Rejea zilizoridhiwa na Serikali ambazo ni  kufanya uchunguzi kwenye Makinikia yaliyopo Bandari ya Dar esSalaam, Bandari Kavu na migodini kwa kupekua na kubaini vitu vilivyomo ndani na kuchukua sampuli za makinikia ili kuzifanyia uchunguzi wa kimaabara.

Hadidu nyingine ni Kufanya uchunguzi wa kimaabara na kubainisha aina, kiasi na viwango vya madini yatakayoonekana katika makinikia kisha kubainisha thamani ya madini hayo,kutumia mitambo ya scanners iliyopo katika Bandari ya Dar esSalaam kwa ajili ya kujiridhisha na aina ya shehena zilizomo kwenye makontena yenye mchanga wa madini.

Kubainisha uwezo wa scanners hizo kuona vitu vyenye ukubwa na maumbile tofauti vilivyomo ndani ya makontena yenye makinikia, kuchunguza utendaji wa Wakala wa Serikali wa Ukaguzi Madini(TMAA) wa kuchukua sampuli za makinikia,uchunguzi wa madini kwenye maabara na utaratibu wa ufungaji wa utepe wa udhibiti (seal) kwenye makontena kabla ya kusafirishwa nje ya nchi.

 Ili kutekeleza uchunguzi huu,Kamati  hiyo ya vita ya kiuchumi katika sekta ya madini ilifanya yafuatayo ,kuandaa mpango kazi, kukusanya nyaraka na taarifa mbalimbali kuhusiana na makontena yenye makinikia yaliyozuiliwa na Serikali kusafirishwa nje ya nchi,kutembelea maeneo yote yenye makontena yenye shehena za makinikia ili kuyachunguza na kuchukua sampuli zake.

Maeneo hayo ni Bandari ya Dar es Salaam, Bandari Kavu – ZAM CARGO na migodi ya Bulyanhulu na Buzwagi,kutathmini uwezo wa scanners wa kuonesha makinikia yaliyomo ndani ya makontena pamoja na vitu vingine ambavyo vinaweza kuwa ndani ya makinikia.

Kamati hiyo ya Rais pia ilifanya uchunguzi wa kimaabara wa sampuli za makinikia na kubaini aina,viwango na kiasi cha madini yaliyomo kwenye makinikia,kukokotoa thamani ya madini yaliyopimwa kwenye makinikia kwa kutumia viwango vilivyopatikana kutokana na uchunguzi wa kimaabara na thamani ya madini hayo kwenye soko la dunia na kuchunguza utendaji wa Wakala wa Serikali (TMAA) wa kukagua na kudhibiti uzalishaji na usafirishaji wa makinikia.

Vita hii ya Rais imezaa matunda ambapo sasa watanzania wameanza kuona neema katika madini yetu,hivyo basi tumuunge mkono Rais katika Vita hii ngumu ya kiuchumi ili hatimaye watanzania waanza kunufaika katika sekta ya madini,gesi na mafuta.

Makala haya yameandikwa na Albano Midelo,baruapepe albano.midelo@gmail.com

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa