• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

VITUO VIWILI VYA TIBA MBADALA VYAFUNGIWA

Tarehe ya kuwekwa: November 11th, 2017

ZIARA ya kushitukiza ikiongozwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dk.Gozibert Mutahyabarwa imefanyika  katika Kliniki za Manispaa ya Songea na kubaini kliniki mbili  zinaendeshwa kinyume cha sheria za tiba asili na tiba mbadala.Baada ya ukaguzi wa kina toka katika timu mbili za wataalam wa Afya ngazi ya Mkoa wa Ruvuma na wa Manispaa ya Songea umebaini vituo vya Ndulu Herbal Clinic kilichopo Mahenge na Bethlehemu Samaritan Clinic  kilichopo  Mfaranyaki Songea  vinapima wagonjwa kwa kutumia  kipimo cha Qantum Resonance Magnetic Analzer ambacho kimepigwa marufuku na serikali.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amesema vituo vyote vya tiba asilia viliandikiwa barua kutoka Manispaa ya Songea kuacha kutumia kipimo hicho ambacho kinawarubuni wananchi kuwa wanaumwa magonjwa mengi hivyo kulipa gharama kubwa kwa ajili ya matibabu ambazo ni kati ya shilingi 150,000 hadi 300,000.Hata hivyo vituo tiba vya asili vimekaidi   na kuendelea kutumia kipimo hicho kupima wagonjwa  ambapo utafiti uliofanywa na madaktari ulibaini kipimo hicho kinatoa vipimo vya uongo na hakina viwango vya ubora.

Licha ya kutumia kipimo ambacho kimepigwa marufuku,mapungufu mengine ambayo yamebainika katika operesheni hiyo ni vituo hivyo kutumia watalaam ambao hawana sifa za kuwa madaktari na wahudumu wa afya ambapo kituo cha Betherehemu Samaritan Clinic hakijasajiriwa.Kutokana na mapungufu hayo vituo hivyo vimefungwa kuanzia leo Novemba 10,2017 na mashine walizokuwa wanazitumia zimechukuliwa na Idara ya Afya Manispaa ya Songea.

Hata hivyo vituo hivyo vinaweza kufunguliwa iwapo vitafanyia marekebisho maagizo ya serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kuzingatia sheria,kanuni na miongozo ili vituo hivyo vitoe huduma rafiki na salama kwa watumiaji.Dk.Mutahyabarwa amesisitiza kuwa kutokana na ukubwa wa tatizo ziara za kushitukiza zitafanyika katika mkoa mzima wa Ruvuma ili kulinda maisha ya wananchi kutokana na matumizi yasiokuwa salama katika tiba asili na tiba mbadala.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa