• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAANDISHI WA HABARI MKOANI RUVUMA WAPEWA MAFUNZO NA TAKUKURU KUKABILIANA NA RUSHWA KUELEKEA UCHAGUZI MKIUU.

Tarehe ya kuwekwa: October 21st, 2020

Uchaguzi mkuu ni jambo la msingi sana katika Taifa letu kwani ndipo tunapopata viongozi wanaobeba dhamana ya kutuongoza katika mapambano ya kiuchumi na jamii ili kuweza kutimiza malengo mbalimbali ya serikali kwa wananchi wake.

Kauli hiyo imetamkwa na Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Hamza Mwenda katika semina kwa waandishi wa habari Mkoani Ruvuma iliyofanyika katika ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma leo 21/10/2020.

Mwenda alisema “lengo la kikao hicho ni kukumbushana mambo mbalimbali yanayohusu rushwa kuhisiana na masuala ya uchaguzi  ambao unatarajia kufanyika tarehe 28 oktoba mwaka huu.”

Alibainisha  kuwa sheria ya uchaguzi namba 6 ya mwaka 2010 ilitungwa kwa madhumuni ya kuweka kwa sheria itakayosimamia na kuratibu mapato na kudhibiti matumizi pamoja na gharama za uchaguzi kwa vyama vya siasa na wagombea ikiwa imeainishwa matendo yanayokatazwa.

Aliongeza kuwa madhumuni ya sheria na kanuni hizo ni pamoja na kudhibiti vitendo vya rushwa wakati wa uchaguzi na kupata viongozi kwa njia ya haki ambapo sheria hizo ni pamoja na katiba ya Jamhuri ya Muunganowa Tanzania yam waka 1977, sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007, sheria ya uchaguzi wa kitaifa namba 1 ya mwaka 1985 na kanuni zake, sheria ya gharama za uchaguzi namba 6 ya 2010, sheria ya mwenendo wa makossa ya jinai sura ya 20, sheria ya ushahidi sura 6, na hukumu za kesi zilikwisha tolewa maamuzi na mahakama.

 Akizitaja sababu za kuwepo kwa rushwa katika uchaguzi ambapo hutofautiana kati ya wapiga kura na wagombea ambazo ni pamoja na wapiga kura- kuwa na tamaa ya kupata kitu chochote chenye kunufaisha bila ya watu wote, uelewa mdogo wa wapiga kura kuhusu haki na wajibu wao katika uchaguzi na umuhimu wa kura zao, umaskini unaosababisha kudai au kupokea rushwa, kukosa uzalendo, mazoea na utamaduni uliojengeka wakati wa uchaguzi ni ni sehemu ya kupata fedha na mmomonyoko wa maadili.

Aliongeza kuwa sababu za  wagombea kutoa rushwa ni pamoja na utamaduni uliojengeka na kutojiamini nafasi aliyogombea kwa kutotoa kitu chochote hatachaguliwa katika uchaguzi, kuhofia  kushindwa katika uchaguzi mkubwa na kutokubali kushindwa, na ukosefu wa maadili.

Hakusita kutaja madhara ya rushwa katika uchaguzi ni kukosa viongozi wazuri ambao ni wazalendo kwa Taifa letu, kupata viongozi wasio wazalendo wanaoingia madarakani kwa rushwa, kupata viongozi ambao wanalenga kurudisha gharama walizotoa kuingia madarakani, kutosimamia kikamilifu kwenye miradi ya maendeleo kutokana na kukosa viongozi wenye uchungu nayo, kudumaa kwa uchumi wa Taifa, kudidimiza haki ya usawa wa kushiika nafasi za uongozi, kudhoofisha demokrasia, kuondoa uhuru wa mpiga kura.

Alisema wajibu wa mwandishi wa habari  katika kuzuia na kupambana na rushwa katika uchaguzi mkuu ni kufanya kazi kwa  uadilifu, kuwa mtu wa  kujielimisha mambo mbalimbali yanayokuzunguka, mwanahabari anawajibika kutoa taarifa ofisi ya TAKUKURU pale aonapo vitendo vya rushwa vinatokea, ni wajibu wake  kukataa kuandika habari zinazokiuka  maadili ya uandishi wa habari, na kushiriki mikutano ya kampeni ili kujua sera za vyama zitakazomwezesha kuchagua kiongozi atakaye wajibika katika jamii.

IMETAYARISHWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

21 OKTOBA 2020.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa