• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAFANYABIASHARA wa Songea kufanya ziara ya mafunzo nchini Poland

Tarehe ya kuwekwa: September 18th, 2018

MBUNGE wa Jimbo la Songea mjini mkoani Ruvuma Dkt.Damas Ndumbaro anawatangazia wakulima na wafanyabiashara  wa Manispaa ya Songea na Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla kuwa safari ya mafunzo ya  nchini Poland inatarajia kufanyika Oktoba 9 mwaka huu.

Kulingana na Mbunge huyo amefanya mazungumzo na Balozi wa Poland kuhusiana na taratibu na Visa tangu Julai mwaka huu na kwamba maandalizi ya safari hiyo yanaendelea vizuri.

Dkt.Ndumbaro amesisitiza kuwa hiyo ni fursa adimu kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma na kwamba wakiwa nchini Poland watajifunza namna nchi hiyo ilivyofanikiwa katika sekta ya kilimo,pia wafanyabiashara wa Mkoa wa Ruvuma watatangaza fursa za kilimo,biashara,utalii na uwekezaji zilizopo katika Mkoa wa Ruvuma.

Hata hivyo amesema wafanyabiashara na wakulima wanaotarajia kwenda katika ziara hiyo ya mafunzo ya siku tano hawazidi kumi  ambao kila mmoja anatakiwa kuchangia nauli kati ya Dola 800 hadi 1000 na  gharama ya malazi na chakula ni kati ya Dola  500 hadi 700.

Mfanyabiashara yeyote ambaye anapenda kwenda katika ziara hiyo anatakiwa kufika katika Ofisi ya Mbunge wa Songea na kuandikisha jina lake kuanzia sasa hadi Septemba 23,2018.Wafanyabiashara hao pia wanatakiwa kuandaa Pasipoti zao za kusafiria kwa ajili ya maandalizi ya VISA.

Nchi ya Poland iliyopo katika Bara la Ulaya inatajwa kuwa ndiyo nchi ambayo inayoongoza katika bara hilo katika uzalishaji wa zao la mahindi ambapo hekta moja inazalisha tani 11 za mahindi.

Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa nchini inayoongoza kwa uzalishaji wa zao la mahindi,hata hivyo changamoto kubwa ni ukosefu wa soko na pembejeo za kilimo hali ambayo inaleta changamoto kubwa kwa wakulima na wafanyabiashara wa mkoa huo.

Mbunge wa Songea mjini Dk.Damas Ndumbaro amesema hali hiyo ndiyo iliyomsukuma Julai mwaka huu kuwaleta watalaam wa kilimo katika Manispaa ya Songea toka nchini Poland wakiongozwa na Kaimu balozi wa Poland nchini Tanzania Dk.Evelina Lubieniecka.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Septemba 18,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa