• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAJASIRIMALI wadogo Manispaa ya Songea wapewa mkopo wa milioni 95 bila riba

Tarehe ya kuwekwa: December 30th, 2018

WAJASIRIMALI wadogo ambao ni wanawake,vijana na makundi maalum katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wamepewa mkopo wa milioni 95 bila riba.

Mkuu wa Idara ya  Maendeleo ya Jamii katika Manispaa hiyo Naftari Saiyoloi  akizungumza katika hafla ya utoaji wa mkopo huo kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea amesema kiasi hicho cha fedha kinatolewa katika vikundi 59 vya wajasirimali hao.

Amesema kati ya vikundi hivyo,vikundi vya wanawake 30 vimekopeshwa zaidi ya shilingi milioni 30,vikundi vya vijana 19,vimekopeshwa zaidi ya shilingi milioni 37 na vikundi maalum 10 vimekopeshwa zaidi ya shilingi milioni  26.

Hata hivyo Saiyoloi amesema katika kipindi cha  mwaka wa fedha wa 2018/2019 kwa robo ya kwanza Manispaa hiyo ilikopesha wajasiriamali wadogo kutoka vikundi 59 kiasi cha shilingi milioni 59.

Kwa upande wake mgeni rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa wilaya ya Songea Pololet Mgema ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kutoa asilimia kumi ya makusanyo ya mapato ya ndani kwa kuzingatia sheria namba 37A(2) iliyoagiza mgao stahili kwa makundi yote.

“Naipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kuwa mstari wa mbele katika kutekeleza maagizo ya serikali katika utoaji wa mikopo hii katika makundi haya’’,alisisitiza.

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Alhaj Abdul Hassan Mshaweji amewaasa wajasirimali wadogo kuirejesha mikopo kwa wakati  ili wakopeshwe wajasirimali wengine.

“Mkopo huu unalenga kupambana na adui umasikini,matajiri wote mnaowaona wakubwa leo wakiwemo Dkt.Mengi na wengineo,walianza kama wajsirimali wadogo na hivi sasa ni miongoni mwa matajiri wakubwa Tanzania’’,alisema Mshaweji.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Songea mjini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt.Damas Ndumbaro amesema amefarijika kuona mabadiliko ya sheria ya fedha namba 37 katika serikali za mitaa kuanza kuwanufaisha wajasiriamali wadogo.

Amesema katika marekebisho ya sheria hiyo yaliofanywa na Bunge mwaka huu,yanamwezesha mjasirimali mdogo wakiwemo wanawake,vijana na makundi maalum kukopeshwa mikopo bila riba.

Halmashauri ya Manispaa ya Songea katika wilaya ya Songea ndiyo Halmashauri pekee kati ya tatu ambayo inatekeleza kwa vitendo sheria ya kutoa mikopo ya asilimia 10 ya makusanyo ya ndani  katika kila robo ya mwaka wa fedha.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Desemba 30,2018.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa