• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANAFUNZI 54,890 Kumeza dawa za Minyoo na Kichocho kwa shule za Msingi Manispaa ya Songea

Tarehe ya kuwekwa: November 17th, 2022

Halmashauri ya Manispaa ya Songea  inatekeleza zoezi la umezeshaji dawa za minyoo  na kichocho kwa wanafunzi wa shule za msingi 96 zilizopo Manispaa ya Songea ambalo linaendeshwa na Walimu wa afya chini ya usimamizi wa  Wataalamu wa afya  kuanzia leo  tarehe 17 hadi tarehe 18 Novemba 2022.

Mratibu Elimu  wa  magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Bload Komba alisema Manispaa ya Songea imeanza zoezi la umezeshaji wa dawa za minyoo na kichocho kwa wananfunzi wa shule ya msingi kuanzia miaka 5 hadi 14  kwa idadi ya wanafunzi 54,890 wakiwemo wavulana 27,426 na wasichana 27,710.

Bload alisema lengo la kutoa dawa hizo ni kwa ajili ya kinga ya  minyoo  tumbo na ugonjwa wa kichocho ambapo mwanafunzi atapimwa urefu kuanzia sentimita 90 ataweza kumeza dawa na endapo atakuwa  chini sentimita 90 au chini ya iaka mitano 5 hatapewa dawa.  

Alisema dawa itakayotolewa kwa wanafunzi ni dawa aina ya  Albendazole - dawa za minyoo ya tumbo na dawa ya kichocho ambayo imeshauriwa kuanza kula chakula kabla ya kumeza dawa.

Aliongeza kuwa dawa hizo ni  kinga na salama na hazina madhara  endapo  zitatumika  kwa usahihi japokuwa yapo baadhi ya maudhi madogo madogo yanayoweza kutokea na ya muda mfupi ikiwemo na kichefuchefu, kuharisha, kichwa kuuma, homa, na maumivu ya tumbo endapo yatatokea maudhi madogo madogo watoe taarifa kwa wataalamu wa afya kwa hatua zaidi .

Akibainisha  Manufaa ya dawa za kinga tiba endapo zitatumika kwa usahihi ni pamoja na kupunguza maambukizi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine, kuua vimelea vya magonjwa hayo, kuepusha upungufu wadamu, kupunguza magonjwa ya ngozi, kuboresha nguvu kazi pamoja na kuwafanya watoto wakue vizuri. “Alibainisha “

Amewataka walimu hao kusimamia zoezi hilo kwa weredi na kuzingatia maelekezo yote yaliyotolewa na wataalamu wa Afya na kuhakikisha wanafunzi walioandikishwa wote wenye umri kuanzia miaka 5 hadi 14  wanapewa dawa za kinga tiba.

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa