• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANAFUNZI WA SHULE ZA SEKONDARI KUSHIRIKI MASHINDANO YA UBUNIFU WA SAYANSI NA TEKNOLOJIA.

Tarehe ya kuwekwa: February 11th, 2021

Manispaa ya Songea ni miongoni mwa Halmashauri nane zilizopo Mkoani Ruvuma ambazo zitashiriki  mashindano ya ubunifu wa Sayansi na Teknolojia kwa wanafunzi wa shule za Sekondari nchini.

Afisa Elimu Sekondari Manispaa ya Songea Devotha Luwungo amesema  Halmashauri ya Manispaa ya Songea ina jumla ya Sekondari 41, kati ya hizo shule za Sekondari 3 ndizo zilizofanya vizuri kwa ubunifu wa vipaji vya wanafunzi ambazo ni Matarawe Sekondari, Zimanimoto Sekondari, na Matogoro Sekondari.

Devotha alieza  kuwa mashindano hayo yatahusishwa na uibuaji wa  vipaji maalumu vya Sayansi na Teknolojia ambapo kwa Manispaa ya Songea  imepata wanafunzi 3 wenye vipaji bora ambao ni  Abdul Omari Msafiri mwanafunzi kutoka shule ya Zimanimoto Sekondari – muundaji wa kifaa kinachotenganisha vimiminika vigumu na laini ( mfano mafuta kutoka kwenye maji) improvised separating funnel,  mwanafunzi Walen John Mbunda kutoka shule ya Sekondari matarawe - uundaji wa magari yanayotumia umeme ( auto mobile), na mwanafunzi Annastasia Leonard Mdogi  kutoka shule ya sekondari ya Matogoro-mchoraji wa picha mbalimbali. 

Naye Mkuu  wa shule ya sekondari Matarawe Francis Sasu alisema mwanafunzi Walen John Mbunda ni mwanafunzi wa kidato cha tatu ambaye  aliwahi kushiriki mashindano ya Majimaji Selebuka mwaka 2020 na alionyesha kivutio cha kipaji kikubwa, na hadi leo hii ameweza kufanya vizuri kwa kubuni uundaji wa gari linalotumia umeme (auto mobile).

Alisema “mara nyingi huwa wanawahimiza wanafunzi kuhusu mitaala ya kawaida na kuwashawishi, kuwashauri juu ya vipaji vyao mbalimbali pamoja na kuwatia moyo ili waweze kukuza vipaji vyao kwa sababu yawezekana mtoto akawa na uwezo mdogo wa kitaaluma darasani lakini akaweza kuwa na kipaji kizuri cha ubunifu”.  Sasu alibainisha.

Nao wanafunzi washiriki wa mashindano hayo, walisema wanaiomba serikali iwasaidie kuwawezesha kuwapeleka kusoma  shule zenye vipaji maalumu ili waweze kuboresha fani zao.

Akizitaja faida za kutumia magari yasiyotumia mafuta ni pamoja na  kuokoa gharama za mafuta, kuondoa uchafuzi wa mazingira (moshi) na nyinginezo. “Alibainisha mwanafunzi Walen John Mbunda.”

 Mashindano hayo yamemalizika kiwilaya na sasa yataendelea kufanyika ngazi ya mkoa na hati;maye kitaifa.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

10.02.2021.

 

 

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa