• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI WA MWENGEMSHINDO KULIPWA FIDIA

Tarehe ya kuwekwa: November 9th, 2017

MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Songea Alhaj Abdul Hassan Mshaweji  amesema serikali imekubali kulipa fidia ya sh.bilioni 3.3 za  ardhi kwa wananchi wa Kata ya Mwengemshindo Manispaa ya Songea.Eneo hilo lenye ukubwa wa zaidi ya hekari 5000 lilichukuliwa na serikali katika mwaka wa fedha wa 2008/2009  kwa ajili ya eneo maalum la ukanda wa uwekezaji viwanda(EPZA).

Akitoa taarifa katika mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Songea Meya Mshaweji ameliambia Baraza hilo kuwa Kamati Maalum ikiongozwa na Mbunge wa Songea mjini,Mstahiki Meya wa Songea na Diwani wa Kata ya Mwengemshindo walikwenda Dodoma na kufanikiwa kukutana na Waziri wa Fedha ambaye aliahidi serikali kulipa fidia hiyo.

Kwa mujibu wa Taarifa hiyo,Waziri wa Fedha ameahidi serikali katika mwaka huu wa fedha wa 2017/2018 italipa fidia ya sh.bilioni 1.5 kwa wananchi wa Mwengemshindo ili kupunguza deni hilo ambalo wananchi wanadai kwa muda mrefu.Wananchi 1181 wa Kata ya Mwengemshindo wanadai fidia ya sh.bilioni 3.3  ambapo  hadi sasa serikali imelipa shilingi bilioni mbili za fidia kwa wananchi hao.

Wakichangia taarifa hiyo baadhi ya madiwani  wameiomba serikali kulipa fidia hiyo haraka kwa kuwa wananchi wamechoka kusubiri  ambapo baadhi ya wananchi wamekufa bila kupata haki yao.Diwani wa Kata ya Mwengemshindo Osimundi Kapinga amesema serikali ilichukua ekari zaidi ya 5000 za wananchi miaka kumi liyopita ambapo hadi sasa fedha za fidia ambazo zimelipwa ni sh.bilioni mbili tu kati ya fedha zaidi ya shilingi bilioni tano ambazo zinadaiwa na wananchi.

Amesema serikali imekuwa inaahidi kila mwaka wa fedha kuwalipa wananchi fidia yao ambapo hadi sasa hakuna utekelezaji hali ambayo imesababisha wananchi,wanadai watachukua ardhi yao na kuanza kuifanyia kazi.“Katika Mkutano Mkuu wa kata uliofanyika hivi karibuni tumeadhimia kuchukua ardhi yetu bila masharti yeyote ili tuweze kuzalisha na kujenga nyumba kwa sababu wananchi wamekata tamaa na kuchoshwa na ahadi ambazo zimeshindwa kutekelezwa’’,alisema Kapinga.

Naibu Meya wa Manispaa ya Songea Yobo Mapunda amekiri kuwa madai hayo ni ya muda mrefu ndiyo maana wananchi wamekata tamaa,hata hivyo amesema anaamini serikali ya CCM ni sikivu italipa madai hayo kabla ya mwaka huu wa fedha kumalizika.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa