• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANAWAKE 30 wanafariki kila siku kutokana na matatizo ya uzazi

Tarehe ya kuwekwa: August 17th, 2019

Mkuu wa wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma Pololet Mgema  amezindua kampeni ya jiongeze tuwavushe salama katika kata ya Ruvuma manispaa ya Songea.

Akizungumza katika uzinduzi huo  Mgema amesema kuwa kampeni ya jiongeze tuwavushe salama ina lengo la kuongeza kasi ya uwajibikaji,kupunguza vifo vya wajawazito  na watoto wachanga katika Manispaa ya Songea.

Mgema amesema takwimu ya vifo kwa mwaka 2015/2016   inaonesha kuwa viwango vitokanavyo na uzazi ni 556 kwa kila vizazi hai 100,000 ambayo ni sawa na wanawake 30 ambao hufariki kila siku nchini kutokana na matatizo ya uzazu..

Takwimu za Manispaa ya Songea kwa mwaka 2018  zinaonesha kuwa kulikuwa na vifo 22 vilivyotokea sawa na 188 kwa kila vizazi hai 100,000.  Kutokana na vifo hivyo  Mkuu huyo wa Wilaya amewaomba wananchi kuongeza nguvu kwa kutekeleza na kusimamia ili kuokoa maisha ya wananchi.

“Maneno basi, hapa ni vitendo tu, hapa ni kazi tu, Mama akivuka salama na nchi imevuka salama.’’,alisisitiza Mgema.

 Naye,Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Dkt. Mameritha  Basike ameyata malengo ya kuzindua kampeni hiyo ya jiongeze tuwavushe salama kuwa ni kutaka kupunguza vifo vya wajawazito, wazazi na watoto wachanga nchini Tanzania.

Mganga huyo amesema madhumuni ya kampeni hii ni kuhamasisha viongozi wa ngazi zote,serikali,viongozi wa Dini,Mashirika yasiyo ya kiserikali,wadau wa maendeleo,Watoa Huduma za Afya,Familia na Jamii kwa ujumla.

Kwa mujibu wa Basike, sababu zinazosababisha vifo kwa wazazi na watoto wachanga, ni kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua ambapo  asilimia 18 ya vifo intokana na kifafa cha mimba  na  asilimia tano,kutoka damu kabla ya kujifungua na ,kushindwa kupumua ni  asilimia 25.2.

Hata hivyo amezitaja changamoto wanazokabiliana nazo kuwa uwelewa  mdogo kwa jamii kuhusu masuala ya Afya ya Uzazi kwa Mtoto,akina mama wanachelewa kuanza kliniki mapema na  uhaba wa magari ya kubebea wagonjwa.

Dkt.Basike ameitaja mikakati madhubuti ambayo wameweka kwa ajili ya kupunguza vifo vya mama na mtoto, kuwa ni  kuimarisha huduma za uzazi wa mpango zikiwemo huduma za ushauri kwa wanawake mara baada ya kujifungua,utoaji wa Elimu ya Afya ya uzazi kwa jamii  na ushirikishwaji wa wanaume katika huduma za uzazi.

Halmashauri ya Manispaa ya Songea ina jumla ya vituo 40 vinavyotoa huduma za Afya,kati ya vituo hivyo Hospitali moja,vituo vya Afya vinne na Zahanati 35    

Imeandaliwa na

Farida mussa

Kitengo cha TEHAMA Manispaa

Agosti 16,2019

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa