• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WATENDAJI wa Kata Manispaa ya Songea wasainishwa mikataba ya lishe

Tarehe ya kuwekwa: July 31st, 2019

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tina Sekambo amewasainisha mikataba ya lishe watendaji wa wata 21 zilizopo katika Manispaa hiyo ili kupunguza tatizo la utapiamlo na udumavu katika Halmashauri hiyo.

Mikataba hiyo imesainiwa kwenye ukumbi wa ofsi ya Mkuu wa wilaya ya Songea na kushuhudiwa na Mkuu wa wilaya hiyo Pololet Mgema.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Tina Sekambo  amesema suala la lishe ni la Kitaifa hivyo amewaagiza watendaji hao waende kutekeleza kwa vitendo ili kupunguza upiamlo  na  udumavu  ambao unachangia umaskini na kuathiri makuzi ya watoto ambao ni Taifa la kesho..

Akizungumza baada ya watendaji hao kusaini mikataba, Mkuu wa wilaya ya Songea Pololet Mgema amesema katika wilaya ya Songea hakuna sababu ya kuwa na utapiamlo na udumavu kwa kuwa wilaya hiyo imezalishsa aina mbalimbali za vyakula yakiwemo matunda ya aina mbalimbali.

“Tunataka  kuondoa udumavu, mtendaji yeyote ambaye hatatimiza wajibu wake, katika kusimamia mikataba ya lishe tutamchukulia hatua”. Amesema Mgema.

Amesema ili suala la lishe liweze kufanyika vizuri  imewekwa mikataba ya usimamizi wa kazi ambayo imesainiwa katika ngazi ya kitaifa, mkoa, wilaya,  na sasa katika halmashauri ambapo watendaji wa kata wamesaini na itasainiwa pia na watendaji wa mitaa yote 95 ya Manispaa ya Songea.

Naye Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya songea Dkt Mameritha Basike ameyataja malengo yanayotekelezwa katika mkataba huo kuwa ni kufanikisha suala la kuboresha hali ya lishe na kupunguza athari za utapiamlo katika jamii na kuhakikisha kuwa jamii kupitia uongozi wa mtaa inashiriki ipasavyo katika kupanga,kutekeleza na kufutilia maendeleo ya utekelezaji wa mpango na afua za lishe.

Basike ameyataja majukumu sita katika upimaji wa utendaji kazi katika kukabiliana na utapiamlo,Kuhakikisha lishe ni ajenda ya kudumu katika vikao vva kisheria vya kamati ya maendeleo ya kata, Kuchochea na kuibua fursa za lishe, matatizo na suluhu za kutatua matatizo ya lishe na kuhakikisha vipaumbele vinajumuisha afua za chakula na lishe, afya, maji safi, usafi wa mazingira na uchangamshi kwa watoto wadogo.

Ameyataja majukumu mengine kuwa ni Kukusanya, kuthamini na kujadili taarifa za lishe kutoka kwenye kaya, Kuhakikisha wadau wa lishe wote waliopo kwenye mtaa wanatambulika na wanawasilisha taarifa zao kwenye kamati ya maendeleo ya mtaa na Kufanya ufuatiliaji wa shughuli za lishe na kutolea taharifa.

Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa mitano inyoongoza kwa udumavu na utapiamlo Tanzania.

Imeandikwa na Farida Mussa

Kitengo cha TEHAMA Manispaa ya Songea

Julai 31,2019

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa