• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WATOTO 25,000 Songea wapewa dawa za minyoo

Tarehe ya kuwekwa: May 28th, 2018

JUMLA ya watoto 25,544 katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wamepata dawa za minyoo sawa na asilimia 67.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za lishe katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Machi mwaka huu kwenye kikao cha kamati ya lishe kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea Afisa Lishe wa Manispaa hiyo Anna Nombo  amesema dawa hizo zimetolewa kwa watoto hao katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Machi mwaka huu.

Amesema katika kipindi hicho jumla ya watoto 17,068 wenye umri chini ya mwaka mmoja katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wamehudhuria kliniki katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Machi mwaka huu.

kati ya hao,watoto 12 ambao ni sawa na asilimia 1.1 walikuwa na uzito chini ya asilimia 60.

Kwa mujibu wa Afisa Lishe huyo watoto 1733 ambao ni sawa na asilimia 5.1 walikuwa na uzito kati ya asilimia 60 hadi 80 na kwamba watoto 31,391 sawa na asilimia 91.8 walikuwa na uzito kati ya asilimia 80 hadi 100.

“Katika kipindi hicho jumla ya akinamama 6469 walihudhuria kliniki,kati yao 1905 walipata madini chuma sawa na asilimia 29.4 na akinamama 1636 walipata dawa za minyoo sawa na asilimia 25.3’’,anasema Nombo.

Hata hivyo amesema katika kipindi hicho jumla ya watoto waliozaliwa hai ni 2966 kati yao watoto 236 walizaliwa na uzito pungufu wa kilo 2.5 sawa na asilimia nane.

Nombo anabainisha Zaidi kuwa katika kipindi hicho watoto 4209 wenye umri wa miezi kati ya sita hadi 11 walitarajiwa kupata nyongeza ya vitamin A,ambapo watoto 6624 ndiyo waliopata nyongeza ya vitamin A sawa na asilimia 157.

Amesema watoto 37,879 wenye umri wa miezi 12 hadi 59walitarajiwa kupata nyongeza ya vitamin A,hata hivyo ni watoto 15,167 sawa na asilimia 40 ya lengo ndiyo walipewa vitamin hiyo.

Kulingana na Afisa Lishe huyo katika kipindi hicho jumla ya watoto wachanga 4518 walizaliwa na kwamba mama zao walipewa unasihi wa umuhimu wa kunyonyesha maziwa ya mama pekee kwa kipindi cha miezi sita ya mwanzo yaani(EBF).

Akizungumzia ukaguzi wa madini joto,Nombo amesema umefanyika katika kata saba kati ya 21 za Manispaa ya Songea ambapo jumla ya kilo 6654 za madini joto sawa na asilimia 99.5 zilizokaguliwa kwenye maduka ya rejareja zilikuwa na madini joto ya kutosha.

Takwimu za Januari hadi Machi mwaka huu zinaonesha kuwa uwiano wa nyumba zenye vyoo bora katika Manispaa ya Songea ni asilimia 83.6,ambapo asilimia 47.7 ya kaya zina sehemu ya kunawia mikono.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Mei 28,2018

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Meya wa Songea Atoa Wito kwa Familia Kuchangia Damu Kuokoa Maisha.

    June 14, 2025
  • Tazama zote

Video

Mbunge Akabidhi Kompyuta 6 na Kufadhili Ukarabati wa Ofisi za Polisi
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa