• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WATUMISHI wa afya Manispaa ya Songea walivyojitolea ujenzi wa kituo cha Afya Kata ya Ruvuma

Tarehe ya kuwekwa: October 15th, 2018

MGANGA Mkuu wa Manispaa ya Songea Dk.Mameritha Basike amewaongoza watumishi wa afya wakiwemo madaktari na wauguzi kujitolea katika mradi wa ujenzi wa kituo cha afya kata ya Ruvuma.

Dk.Basike amewapongeza watumishi hao kujitoa na kuwaasa wakazi wa kata ya Ruvuma na manispaa ya Songea kuwa na moyo wa kujitolea ili kuhakikisha ujenzi huo unakamilika kwa wakati.

Jumla ya shilingi milioni 400 zinatarajiwa kutumika katika mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya Kata ya Ruvuma Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Musa Willison ni Mhandisi wa Ujenzi ambaye anasimamia ujenzi wa kituo hicho cha afya ambapo amesema hatua ya ujenzi hadi sasa imefikia asilimia 15 na kwamba wanatarajia kukamilisha hatua za awali za ujenzi huo Januari mwaka 2019 ambapo ametoa rai kwa wakazi wa kata ya Ruvuma kuwa na moyo wa kujitolea ili ujenzi huo uweze kukamilika kwa wakati.

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Alhaj Abdul Hassan Mshaweji ameishukuru serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt.John Magufuli kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho ambao amesema ukikamilika utasogeza huduma ya afya jirani na wananchi.

Akitoa taarifa ya mapokezi ya fedha shilingi milioni 400,Mganga Mkuu wa Manispaa ya Songea Dk.Mameritha Basike amesema fedha za ujenzi wa mradi huo zitatumia mwongozo uliotolewa na TAMISEMI ikiwemo utaratibu wa kutumia force account ili kupunguza gharama za ujenzi wa mradi.

Kwa mujibu wa mwongozo  wa matumizi ya fedha zinazopelekwa Halmashauri kwa ajili ya ukarabati au ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya nchini,fedha hizo zimelenga kukarabati vituo au kujenga katika maeneo ya vipaumbele.

Dk.Basike anavitaja vipaumbele vilivyowekwa katika mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya cha Ruvuma kuwa ni jengo la upasuaji,wodi ya akinamama,wodi ya watoto, maabara, nyumba ya mtumishi inayojitegemea na chumba cha kuhifadhia maiti.

“Mradi wa kituo cha Afya Kata ya Ruvuma mkataba wake unaanza Julai hadi Novemba 2018,ili kufanikisha ujenzi huo,kamati tatu zinahusika kusimamia ambazo ni Kamati ya Ununuzi,Kamati ya Mapokezi na Kamati ya Ujenzi’’,alisema Dk.Basike.

Kwa upande wake Dkt.Zainab Chaula kwa niaba ya Katibu Mkuu TAMISEMI  amewaagiza wakurugenzi nchini kuhakikisha kuwa fedha za ukarabati au ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za Afya  hazitumiwi kinyume na malengo na matarajio yaliyokusudiwa na kwamba fedha hizo ziingizwe kwenye mipango ya fedha za maendeleo.

Naye Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Seleman Jafo ametoa miezi mitatu kwa waganga wakuu wa mikoa nchini,kuhakikisha wanakamilisha miradi ya ujenzi wa vituo vya afya na vituo vipya kujengwa.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa