• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZABUNI WASHAURIWA KUSAMBAZA MAHINDI LISHE SHULENI KWA LENGO LA KUBORESHA AFYA ZA WANAFUNZI

Tarehe ya kuwekwa: April 27th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

27 APRILI 2022

Kamati ya lishe Halmashauri ya Manispaa ya Songea yajipanga kuhamasisha jamii kutumia mazao lishe kwa lengo la kudhibiti utapiamlo na udumavu katika jamii.

Hayo yamebainishwa katika kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa shughuli za lishe Manispaa ya Songea kwa kipindi cha robo ya tatu ya mwaka 2021/2022, kilichofanyika leo tarehe 27 Aprili 2022 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Manispaa ya Songea, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Christopher Ngonyani (Mratibu Tasaf Manispaa ya Songea), alisema kuwa kamati ya lishe imejipanga kutoa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa matumizi ya maziwa kupitia vyombo vya habari pamoja na mikutano mbalimbali inayofanyika katika ngazi ya Kata na Mitaa.

Aliongeza kuwa, kupitia maadhimisho ya siku ya wakulima (Nane Nane) inayotarajiwa kufanyika tarehe 8 Agosti 2022, kamati ya lishe imejipanga kutoa elimu ya namna ya uzalishaji mazao lishe kama vile mahindi ya njano, viazi lishe na mchicha lishe kwa jamii pamoja na umuhimu wa kutumia mazao hayo katika kuboresha afya na kudhibiti utapiamlo na udumavu hasa kwa watoto walio na umri chini ya miaka 5.

Ngonyani ametoa rai kwa wazazi kuhakikisha watoto wanapata chakula chenye virutubisho lishe  wanapokuwa shuleni pamoja na kuwataka wazabuni wanaosambaza chakula mashuleni kupeleka chakula chenye viini lishe hasa kutumia mahindi lishe ili kuimarisha afya za watoto hao.”Alisisitiza”

Akitoa tathimini ya utekelezaji wa shughuli za lishe, Afisa lishe Manispaa ya Songea Florentine Kissaka amesema kuwa hali ya lishe kwa Manispaa ya Songea inazingatia viashiria mbalimbalia ambapo hadi sasa idadi ya watoto wenye umri chini ya miaka 5 wenye utapiamlo mkali imefikia watoto 21 sawa na asilimia 0.2% na asilimia 6.6% ya watoto waliozaliwa na uzito pungufu pamoja na asilimia 35.3% ya watoto wenye udumavu.

Kissaka ametoa wito kwa jamii kuzingatia taratibu za kiafya na utumiaji wa lishe bora zinazotolewa na wataalamu wa afya ngazi ya jamii na katika vituo vya afya ili kukabiliana na utapiamlo na udumavu hasa kwa watoto walio na umri chini ya miaka 5.

Amewataka akinamama wanaonyonyesha kuzingatia maelekezo wanayopewa na watoa huduma katika vituo vya afya ikiwemo na kunyonyesha mtoto chini ya miezi 6 pasipo kumlisha chakula cha aina nyingine na baada ya muda huo kumpatia mtoto chakula cha ziada chenye virutubisho lishe ili kuepukana na tatizo la udumavu na utapiamlo.

“Miongoni mwa mikakati iliyowekwa katika kukabiliana na utapiamlo na udumavu katika jamii ni kuhakikisha ulimaji wa bustani za mbogamboga pamoja na upandaji wa miti ya matunda katika maeneo ya shule pamoja na kutoa elimu ya maandalizi ya chakula lishe shuleni” Kissaka alibainisha.

Naye Afisa kilimo Msaidizi  Manispaa ya Songea Claudy Yacent Massawe alisema kuwa Mkoa wa Ruvuma unafanya vizuri katika eneo la uzalishaji wa chakula ambapo hadi sasa hali ya uzalishaji wa mazao ya chakula inafikia Tani Laki moja na hamsini elfu ambapo Tani sitini na nane elfu pekee hutumika kwa chakula.

Massawe amewataka wakulima kujikita kwenye kilimo cha mazao lishe hasa mahidni ya njano na viazi lishe kwa lengo la kuondoa changamoto ya utapiamlo na udumavu katika jamii.

Kwa upande wake mdau wa kamati ya lishe Manispaa ya Songea Agrey Kapinga amesisitiza utoaji wa elimu kwa jamii juu ya utumiaji wa mazao yanayozalishwa kwa mfumo wa lishe bora pamoja na namna ya uandaaji wa vyakula mbalimbali kwa kuzingatia taratibu zinazotakiwa.

Mwisho.  

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa