• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZEE waiomba serikali kupewa vitambulisho vya matibabu

Tarehe ya kuwekwa: October 2nd, 2019

Mwenyekiti wa Wazee Mkoa wa Ruvuma katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Alezian Nyoni amefurahishwa na kitendo cha wazee kujikita kwenye ujariamali baada ya kustaafu.

Akizungumza na wazee katika uwanja wa Zima moto mjini Songea, Nyoni amesema wazee kujishughulisha na biashara mbali mbali kunawasaidia kuimalisha afya zao na kuwasihi wazee kwenda kupima afya zao mara kwa mara ili kutambua magonjwa ambayo yanawasumbua.

“Safari ya kuelekea uzeeni haina budi kuwa na usawa na haki kwa sababu uzee haukwepeki kwa mtu yeyote leo utakuwa kijana ila kesho utakuwa mzee kwa hiyo tuwaheshimu wazee kwa maana wamefanya mengi katika kuchangia Taifa letu’’,alisisitiza.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo  Sophia Mfaume Kizigo amesema wazee wanaishi muda mrefu kutokana huduma za afya kuboreshwa  katika uongozi wa awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt.John Magufuli.

Kizigo amesema  amesema ni vizuri wazee kwenda kuchukua vitambulisho vya ujasiriamali ili kuepuka usumbufu na kwamba  Rais  ameona ni vyema kuwasaidia wajasiriamali waweze kuepukana na kero ya kulipa mapato makubwa kwenye Halmashauri.

Kwa upande wake Afisa Ufuatiliaji na Tathimini wa  PADI Simon Komba amesema Taasisi yao ni kusaidia masikini na wasiojiweza kama kutoa mikopo ya fedha mifugo pia kutoa elimu ya ujasiriamali kwa wazee na kuwajengea uwezo wa kufuatilia haki zao katika sekta mbali mbali.

Komba amesema PADI wanawaunganisha wazee kwenye taasisi mbali mbali za kifedha kama bajeti ya kuwawezesha  wazee wanawake kiuchumi kwa kuwapa mikopo kwa ujumla wa wazee wote.

Mzee Boniventula  Ngonyani miaka 75 amesema mkazi wa mjimwema  amefurahishwa na Serikali kuweka siku ya wazee duniani ingawa amesema  kuna changamoto  zinazowakabili wazee ikiwemo  upatikanaji wa mbolea na  matibabu kwa wazee.

“Naiomba  Serikali ya awamu ya Tano iendelee kutafutia changamoto mbalimbali zinazowakabili wazee wa Tanzania’’,alisema Ngonyani.

Mzee Bernadetar Hyera miaka 61 mkazi  ameiomba serikali kuwakumbuka wazee ambao wamesahaulika katika huduma za afya.

Imeandikwa na Farida Mussa

Kitengo cha TEHAMA Manispaa ya Songea

Oktoba 2,2019 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa