• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI Mkuu awaagiza wakurugenzi wa Halmashauri kufuatilia utendaji kazi wa watumishi wa umma

Tarehe ya kuwekwa: January 4th, 2019

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini wafuatilie utendaji kazi wa watumishi kwenye maeneo kubaini kama wanakwenda kwa wananchi na kuwahudumia ipasavyo.


‘Serikali inahitaji kuona watumishi wa umma wanakwenda kwa wananchi  kusikiliza kero na changamoto mbalimbali zinazowakabili ili kushirikiana nao katika kuzipatia ufumbuzi’’.


Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana (Alhamisi, Januari 3, 2019) wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Lugagala, wilayani Songea akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Ruvuma.


“Rais wetu Dkt John Magufuli ni muumini wa maadili na mchapakazi ,ndio maana amesisitiza umuhimu wa watumishi wa umma kwenda kuwahudumia wananchi katika maeneo yao, kwani baadhi yao hawana uwezo wa kufikia maeneo ya kutolea huduma.”


Waziri Mkuu aliongeza kuwa ni vema kwa watumishi wa umma wahakikishe wanapanga muda wa siku tatu kwa wiki kutoka maofini kwenda kuwahudumia wananchi hususani waishio maeneo ya pembezoni.


Alitumia fursa ya mkutano huo kuwataka wananchi waendelee kuiamini Serikali yao pamoja na watendaji wake waliopo kwenye maeneo mbalimbali nchini kwani Serikali inatambua matatizo yao na kuahidi kuwa yatapatiwa ufumbuzi kwa wakati.


Waziri Mkuu aliongeza kuwa Serikali haina msamaha na watumishi wazembe, hivyo wananchi waendelee kuwa watulivu na imani kwani watahudumiwa na ahadi zote zilizotolewa na Rais Dkt Magufuli katika maeneo yao zitatekelezwa.


Kadhalika, Waziri Mkuu alimuagiza Mkuu wa Wilaya ya Songea asimamie zoezi la kuwaondoa wananchi wote wanaoishi na kufanya shughuli za kibinadamu ikiwemo kilimo katika maeneo ya vyanzo vya maji kwa sababu watasababisha vyanzo hivyo vikauke.


Awali, Waziri Mkuu aliweka jiwe la msingi katika mradi wa maji wa Luyehela kwenye kijiji cha Muungano Zomba, kuzindua kituo cha kuchotea maji cha kijiji cha Lugagala na kukagua mradi wa ujenzi ya zahanati wa kijiji hicho.


Mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenister Mhagama ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Peramiho na Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga.


Wengine ni Naibu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, Naibu Waziriwa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme na maafisa wengine wa Serikali.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa