• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO AMEWATAKA MAAFISA HABARI KUTANGAZA MIRADI YA SERIKALI.

Tarehe ya kuwekwa: May 24th, 2021

“Utoaji wa taarifa kwa umma ni Takwa la Kisheria, Viongozi wa Umma na Maafisa Habari Tuwajibike”

Ni kauli mbiu iliyotolewa katika mkutano wa 15 wa kikao kazi cha maafisa habari, Mawasiliano na uhusiano wa Serikali  kinachofanyika Jijini Mbeya kuanzia leo tarehe 24 hadi 28 Mei 2021  katika ukumbi wa chuo  kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya “MUST” na kuhudhuriwa  na Maafisa Habari 370  ikiwa kati ya hao Maafisa Habari 20 kutoka Zanzibar.

Mgeni rasmi katika kikao kazi  cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano wa Serikali, Mhe. Innocent Bashungwa ambaye ni Waziri wa Habari, Utamaduni, na michezo,  na kupokelewa na katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Dkt. Hassani  Abbas pamoja  na Sektariet ya TAGCO na kisha kukagua vibanda vya maonesho mbalimbali chuoni hapo  na kupata maelekezo ya huduma zitolewazo katika eneo hilo.

Bashungwa alisema lengo kuu la kikao kazi cha maafisa Habari,  Mawasiliano na uhusiano wa Serikali limejikita katika kutekeleza kauli mbiu ambayo ni utoaji wa taarifa kwa  umma ni takwa la kisheria, Viongozi wa umma na Maafisa Habari tuwajibike,”  ambapo miongoni mwa  mambo ambayo Serikali inasimamia ni pamoja na namna ya utaoaji habari kwa jamii.

Alisema moja ya kazi ya Afisa habari wa Serikali ni pamoja na  kutangaza Miradi  ya Serikali,  kazi zote zilizotekelezwa na Serikali ili kuihabarisha umma iweze kufahamu jitihada zilizofanywa na Serikali yao.

Amezitaja baadhi ya changamoto zinazokwamisha utendaji kazi wa Maafisa Habari ni kutoshirikishwa kwenye vikao mbalimbali vya Taasisi,  kutotengewa bajeti ya Habari na Mawasiliano,  kukosa bando la internet, kutokuwa na vifaa au vitendea kazi vyenye ubora.

Amewataka Waajiri wote nchini kutenga bajeti ya ununuzi wa vifaa bora vya Afisa habari kama Kompyuta, Kamera, vinasa sauti,   ili aweze kufanya kazi kwa kiwango kinachostahili ikiwemo na  upatikanaji wa picha nzuri  za miradi ya Serikali zenye kiwango pamoja na kutengewa bando la internet kwani Afisa Habari mara nyingi  huendelea kufanya kazi wakati wowote  hata nje ya ofisi na baada ya masaa ya kazi. Mhe. Bashungwa alisisitiza.

Ametoa wito kwa Viongozi wote kuhakikisha wanatatua changamoto zote zinazokikabili kitengo cha Habari na Mawasiliano ili kuwezesha jamii kupata habari sahihi, na kwa wakati sahihi na zenye tija kwa jamii na Serikali.

Amesema pamoja na uwepo wa changamoto za ukosefu wa vitendea kazi amewataka  Maafisa Habari hao kuendelea kufanya kazi kwa kujituma kwani anatambua uwepo wa baadhi ya maafisa habari ambao hawajitumi kufanya kazi kwenye maeneo yao kwa kigezo hawana vitendea kazi.

 Ameshauri wasimamizi wa mfumo  wa EGA kwa kipindi kijacho kufuatilia Maafisa Habari  ambao wanafanya kazi vizuri kwenye Website zao wachukuliwe majina yao ili  waweze kupata zawadi ya kufanya kazi vizuri na zenye tija kwa jamii na serikali.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera amewataka maafisa habari wote kuwa makini katika kusikiliza maelekezo yanayotolewa na wawezeshaji hao ili yaweze kuwasaidia katika kuboresha utendaji wa kazi na kutangaza miradi yote ya Serikali.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

24.05.2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa