• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO MH. INOCENT BASHUNGWA ASISITIZA KUWAENZI MASHUJAA WA VITA VYA MAJIMAJI.

Tarehe ya kuwekwa: February 27th, 2021

MAADHIMISHO ya mashujaa wa vita vya Majimaji  Mkoani Ruvuma hufanyika kila mwaka ifikapo tarehe 27 februari kwa ajili ya kuwaheshimu na kuwaenzi mashujaa  vinara wa vita  vya majimaji ambao  walinyongwa na wakoloni ya wakijerumani kwa lengo la kutengua nguvu za upinzani kutoka kwa waafrika ili kuzima vita.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassimu Majaliwa (MB) ambaye aliwakilishwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Inocent Bashungwa (MB) iliyofanyika 27 februari 2021  katika eneo la Makumbusho ya vita vya Majimaji Manispaa ya Songea.

Mh. Bashungwa alisema lengo la Serikali ni kulinda  na kutunza uhifadhi wa maeneo hayo ya kihistoria pamoja na kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa maeneo hayo ya kihistoria ya urithi wa ukombozi wa Afrika.

Alisema  miongoni mwa mashujaa wa vita vya Majimaji ambao  walizikwa katika kaburi moja  wapatao 66 kati ya hao alikuwepo mwanamke mmoja   mwenye cheo cha Nduna ambaye aliitwa Mkomanile. Hivyo alitoa wito kwa wanawake wote siku ya maadhimisho ya wanawake Duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo tarehe 08 machi kila mwaka akumbukwe mwanamke shujaa  Mkomanile ambaye alipigana vita hadi kufa. Alisisitiza.

Aidha katika ziara hiyo aliweza kutembelea kambi ya  Masonya iliyopo Wilayani Tunduru iliyotumika kwa ajili ya mafunzo ya jeshi iliyotumiwa na wapigania uhuru wa chama cha FRELIMO-Msumbiji, Likuyu Sekamaganga- shule iliyotumika kutolea mafunzo kwa watoto wa wapigania uhuru Msumbiji iliyopo Wilaya ya Namtumbo pamoja na maadhimisho ya vita vya Majimaji iliyopo Manispaa ya Songea.

Naye Mhifadhi wa Makumbusho ya Majimaji Mkoa wa Ruvuma Adson Ndyanabo alisema eneo la kihistoria la Mashujaa na vinara  wa vita vya majimaji wapatao 67 walinyogwa tarehe 27.02.1906 wakati wa vita vya majimaji ikiwa ni mbinu mojawapo ya Serikali kikoloni ya wajerumani na kutengua nguvu kwa ajili ya kuzima vita.

Aliongeza kuwa watu wote walioshiriki mapambano walikamatwa kutoka sehemu mbalimbali za Mkoa wa Ruvuma kwa nyakati tofauti kuanzia novemba 1905 hadi 1906 na kuwekwa gerezani wakisubibili na kunyongwa ambapo kaburi kubwa lilichimbwa mwezi mmoja kabla ya siku ya kunyongwa na kazi hiyo ilifanywa na wafungwa hao”mashujaa”.

Alisema Zilisimikwa nguzo ndefu mbili na kuwekwa mwamba juu ya nguzo na  kufunga vitanzi vya Kamba vinne  katika mwamba na chini ya mwamba huo mkubwa zilisimikwa nguzo fupi nne na juu ya nguzo hizo fupi 2 ziliwekewa mwamba kwa juu.

Alibainisha kuwa kabla ya kunyongwa mashujaa hao walibatizwa, kisha wanyongwaji waliletwa kwenye eneo la unyongaji kila mnyongwa akiwa amefungwa mnyororo shingoni na kuvishwa kishuka kiunoni ili kufunika miili yao na kufungwa kitambaa chekundu ili wasione huku  mikono yao ikifungwa nyuma ya mgongo kisha walivishwa kitanzi shingoni na kuning’inizwa vitanzi na kila kitanzi kwa mnyongwa mmoja.

Alisema siku ya kwanza walinyongwa 40 na kisha walizikwa kwa kulazwa kiubavu katika kaburi moja la alaiki la mashujaa 66 akiwemo mfalme (NKOSI) jamii ya wangoni aliyeitwa Mputa Wazerapasi Gama  na kaburi la pili alizikwa Nduna Songea.

Adson alisema  nguvu kubwa ya upinzani ilitokana na uongozi thabiti wa wangoni Nkosi (mfalme) na Nduna ambaye alikuwa na  nafasi ya wasaidizi wa Mfalme na majemedari wa vita pia jumbe ni nafasi ya viongozi wa vijiji walioandikwa na raia walikuwa wapiganaji ambao hawakuwa na vyeo vikubwa.

 Mnara huo ulijengwa 1980 kwa ajili ya kuheshimu,na kutunza  mchango wao wa uzalendo wa mashujaa katika kupigania uhuru.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

27.02.2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa