• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI wa Kilimo na Umwagiliaji Hussein Bashe amewataka Maafisa kilimo kutumia Pikipiki Walizopewa kwa kuwatembelea Wakulima Mashambani.

Tarehe ya kuwekwa: January 17th, 2023

Waziri  wa  Kilimo  na Umwagiliaji  Mhe. Hussein Bashe,  Amewataka  Maafisa Ugani  kutekeleza wajibu wao ipasavyo   ikiwemo na  kuwatembelea Wakulima katika  maeneo  wanayolima ili  kutatua  changamoto mbalimbali  zinazowakabili wakulima  Mkoani Ruvuma.

Hayo yametamkwa katika mkutano wa wadau wa kilimo Manispaa ya Songea uliofanyika tarehe 16 Januari 2023 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea ambao ulishirikisha viongozi ngazi ya Mkoa, Wilaya, viongozi wa vyama vya siasa na wadau wa kilimo kwa lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.

Mhe. Bashe, Alisema kuwa  Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanikiwa kutoa Mbolea ya Luzuku  kwa Mkulima ambayo inauzwa kwa  Bei elekezi ya Luzuku  iliyopangwa na Serikali   kwa lengo la   kuwasaidia Wakulima waweze kuondokana na adha ya Mbolea kuuzwa kwa bei ya juu.

Alisema kwa mwaka 2022 Mkoa wa Ruvuma ulikuwa na Hekta za kilimo 530,000,  Tan za Mbolea  32,000, kwa mwaka 2023 Mkoa wa Ruvuma hadi hivi sasa  umepokea mbolea Tan 42,000 kwa   Hekta za kilimo  930,000.

Amewataka Mameneja wa Makampuni, TFRA, na Mawakala wa Pembejeo  kufanya kazi kwa weredi na uadilifu katika kutoa huduma bora kwa wananchi na kuepuka udanganyifu unaofanywa na baadhi ya wafanyabiashara katika usambazaji na uuzaji wa Pembejeo za kilimo na endapo   atabainika mtu yeyote  anakwenda kinyume na taratibu zilizowekwa atafutiwa Uwakala. “ alisisitiza”

Aliongeza Serikali imejipanga vizuri katika zoezi la usambazaji wa pembejeo,  na amewatoa hofu wakulima wote Nchini  juu ya uapatikanaji wa pembejeo kwa kila mkulima aliyesajiliwa lazima atapata pembejeo  lakini kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Serikali.

  Akizungumza kwa niaba ya wakulima  ndugu Batazari  Mjinga Mkulima wa kijiji cha Mhalule alianza kwa kutoa shukrani za dhati kwa  Rais  wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha Mfumo  mpya wa kidigiti ambao unawasaidia Wakulima   kupata  mbolea ya Luzuku  50%  ambao ni Mkombozi wa Mkulima.

 

Imeandaliwa na;

AMINA PILLY

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.

 

 





Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa