• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wizara ya Afya yapambana na Maradhi yatokanayo na Magonjwa yasiyopewa kipaumbele nchini Tanzania

Tarehe ya kuwekwa: September 16th, 2020

Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii,  Jinsia, Wazee na Watoto imekusudia kuanzisha na kuendeleza Mpango wa pamoja (jumuishi) wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi  kipaumbele kama (ugonjwa wa minyoo ya tumbo na minyoo ya kichocho)   katika Wilaya zote zilizoathirika na magonjwa hayo nchini Tanzania.

Kauli hiyo imetolewa jana 15.09.2020 na Mratibu wa magonjwa yasiyopewa  kipaumbele Manispaa ya Songea Dr. Broady Komba  kwenye kikao cha  Maafisa watendaji wa kata 21, Wenyeviti wa Mitaa 95  pamoja na wataalamu Sekta ya Elimu Msingi kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Broady alisema lengo kuu la Serikali ni kupunguza maradhi yatokanayo na magonjwa yaliyokuwa hayapewi kiupaumbele nchini Tanzania ili kufikia kiwango ambacho si tatizo la afya kwa jamii pamoja na kuhakikisha jamii inakuwa na afya bora na isiyodhoofishwa na maradhi.

Alisema Manispaa ya Songea inakusudia kugawa dawa za minyoo ya tumbo na minyoo ya kichocho kwa wanafunzi wa shule za Msingi 91 za Manispaa ya Songea, kwa idadi ya wanafunzi wapatao 58,000  kwa wanafunzi wenye umri kuanzia miaka 5-14.

Alifafanua kuwa zoezi hilo linatarajia kufanyika  kuanzia  siku ya ijumaa na  jumatatu  yaani 18-21/2020  kwa usimamizi wa walimu wakuu wa shule husika pamoja na wataalamu wa afya ili kuhakikisha dawa hizo  zinagawiwa vizuri  kwa kila mwanafunzi aliyeandikishwa shule hapo.

Aliwaasa Wenyeviti wa mitaa pamoja na vyombo vya Habari kuendelea  kutoa elimu kwa  jamii/ wazazi / walezi  ili waweze kuwapatia watoto wao  chakula cha kutosha kabla ya  kumeza dawa hizo ili ziweze kufanya kazi vizuri bila kuleta tatizo lolote.

Alizitaja faida za kutumia dawa hizo ni  kuwa na mtoto mwenye afya bora, kuwa na utimamu wa akili na kuongeza ufaulu mzuri wa mtoto pamoja na  husaidia kuondoa maradhi ya kifafa.

 Hakusita kuzitaja baadhi ya dalili ambazo zinaweza kujitokeza kwa mtu  aliyekunywa dawa hizo ni  kutapika, kuhisi kichefuchefu, na kulegea  lakini alisema kuwa  dalili hizo zisiwatie hofu kwani hujitokeza mara chache,  na tatizo likizidi mtoto huyo atapelekwa kituo cha afya kilichojirani kwa msaada Zaidi.

Aidha baada ya maelekezo hayo kwa Wenyeviti wa Mitaa na Watendaji wa Kata, yatatolewa tena maelekezo kwa Wakuu na walimu wa afya wa  shule za  Msingi zote ili kuwajengea uwezo wa kiutendaji Zaidi.

IMETAYARISHWA NA;

AMINA PILLY, 

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

16.09.2020

  

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa