• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJILI KATIKA TAMASHA LA KUENZI MCHANGO WA FILAMU YA 'THE ROYAL TOUR' MKOANI RUVUMA.

Tarehe ya kuwekwa: August 16th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

15 AGOSTI 2022.

Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Umma na utawala bora Mhe. Jenista Joackim Mhagama ameongoza wananchi wa Mkoa wa Ruvuma katika Tamasha la kuenzi mchango wa filamu ya ‘The Royal Tour’ kwa shughuli za utalii na uwekezaji Mkoani Ruvuma.

Tamasha hilo limefanyika hapo jana Agosti 16, 2022 katika uwanja wa Majimaji uliopo ndani ya Manispaa ya Songea na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali pamoja na wadau wa utalii kutoka ndani na nje ya Mkoa wa Ruvuma.

Akizungumza kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mhagama ametoa pongezi kwa viongozi wa Mkoa wa Ruvuma kwa kuendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali katika kukuza sekta ya utalii na uwekezaji nchini kwa kuandaa tukio la tamasha hilo.

Waziri Mhagama aliongeza kuwa Filamu ya ‘The Royal Tour’ imelenga kutangaza duniani vivutio vya utalii vinavyopatikana nchini Tanzania ambapo imechangia kwa kiasi kikubwa katika kukuza sekta ya utalii kwa kuongeza idadi ya watalii kutoka nje ya Tanzania na kusaidia kuongeza thamani na uchumi wa pato la Taifa kwa ujumla.”Alibainisha”

Ametoa rai kwa viongozi wa Mkoa wa Ruvuma kuendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ili kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi pamoja na kuimarisha sekta ya madini ambayo inaongoza katika ujenzi wa uchumi wa Mkoa wa Ruvuma.

Waziri Mhagama amewakumbusha viongozi wote Mkoani Ruvuma kutengeneza mifumo ya kitehama kwa kuongeza wigo wa ukusanyaji wa mapato yatakayosaidia kuboresha miundombinu ya uwekezaji.

Pia, amewataka viongozi kusimamia vyema ujenzi wa miundombinu ya elimu, afya, maji na umeme ili kuleta uchochezi wa uchumi endelevu katika Mkoa wa Ruvuma.’Alisisitiza’

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas alisema kuwa lengo la Tamasha hilo ni kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha sekta ya utalii pamoja na kuonyesha vivutio vilivyopo Mkoani Ruvuma.

Ametoa rai kwa wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi kutumia fursa ya uwekezaji iliyopo Mkoani Ruvuma ikiwemo na kilimo pamoja na kutembelea vivutio vilivyopo ikiwemo na Hifadhi ya Taifa ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Ziwa Nyasa, Jiwe Mbuji pamoja na chanzo cha mto Ruvuma kilichopo kwenye Mlima wa Matogoro.

Aidha, Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema ametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kujitoa katika kukamilisha  uandaaji wa mradi wa filamu ya ‘The Royal Tour’ ambayo imeleta mafanikio makubwa nchini.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Ruvuma Oddo Mbunda ameishukuru Serikali kwa kutoa Mbolea ya Ruzuku kwa wananchi wake ambayo itasaidia ongezeko la uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara Mkoani Ruvuma.

Tamasha hilo liliambatana na shughuli mbalimbali ikiwemo na kutembelea chanzo cha mto wa Ruvuma kilichopo katika Mlima wa Matogoro ndani ya Manispaa ya Songea pamoja na burudani za ngoma za asili na wasanii mbalimbali.

Mwisho.

 

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bil. 22.9 Kujenga Masoko ya Kisasa Manzese A na B, na Kiwanda cha Kuchakata Mazao ya Nafaka Lilambo

    July 06, 2025
  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Tazama zote

Video

Makabidhiano ya Mkataba Soko la Manzese A&B
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa