• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJILI KIKAO KAZI " UTOAJI WA CHAKULA SHULENI"

Tarehe ya kuwekwa: June 6th, 2023

MKUU wa Wilaya ya Songea Wilaman Kapenjama Ndile amewataka Viongozi wa Serikali za Mitaa/kata kusoma taarifa ya mapato na matumizi  kwa kila robo ya mwaka ili kuweka uwazi na uwajibikaji kwa wananchi wanaowaongoza.

Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 pamoja na marekebisho yake, Ibara ya 145 na 146, Serikali za Mitaa ni vyombo vya wananchi ambavyo vipo katika ngazi ya chini ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambavyo huundwa, huendeshwa, husimamiwa na kuwajibika kwa wananchi wenyewe ambapo huwezesha wananchi kuwa na Sauti katika maamuzi mbalimbali kwa kushiriki moja kwa moja au kupitia wawakilishi wao katika shughuli za maendeleo na utawala.

Kwa kuzingatia  hilo Serikali ya Mtaa kupitia Mwenyekiti wa Mtaa inao wajibu  kutoa taarifa za mbalimbali za maendeleo ya mtaa husika ikiwemo na kusoma mapato na matumizi ya fedha zilizopokelewa kupitia mkutano wa hadhara kwa lengo la kuweka uwazi na ushirikishwaji  jamii na endapo hatatoa taarifa ya Mapato na Matumizi anaweza kushitakiwa kwa mujibu sheria.

Hayo yamejili katika kikao kazi cha Maafisa Watendaji wa Mitaa 95, Wenyeviti wa Mitaa 95, Watendaji wa kata 21, kamati ya Ulinzi na usalama, pamoja na Wakuu wa idara na Vitengo kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea tarehe 03 Mei 2023 kwa lengo la kuwakumbusha majukumu yao watendaji na wenyeviti wa mitaa katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

Mhe. Ndile alisema Serikali  ikitoa maagizo hayana budi kutekelezwa hivyo amewataka Viongozi hao kuhakikisha wanasimamia suala la mzazi  kuchangia  chakula cha shule kwa shule za msingi na Sekondari ifikapo julai  2023  kwa lengo la kuinua ufaulu wa wanafunzi.

Aliongeza kuwa ili kufanikisha zoezi hilo kila mtaa unatakiwa kuitisha vikao vya kamati za Serikali za Mtaa, mikutano ya hadhara, Bodi za shule pamoja na kamati za shule ili kuweka mkakati bora wa utekelezaji na usimamizi wa michango kutoka kwa wazazi ikiwemo na kufungua akaunti na utunzaji wa chakula.

Hali halisi ya utoaji wa chakula shuleni  Wilaya ya Songea kwa Halmashauri ya Madaba ni 96%, Halmashauri ya Wilaya ya Songea ni 97% ana Halmashauri ya Manispaa ya Songea ni 67%. Mhe. Ndile “ Alibainisha.”

Kwa upande wake Afisa utumishi Manispaa ya Songea Sadiki Mrisho akiwakumbusha majukumu ya Wenyeviti na Maafisa watendaji wa mtaa aliserma  Mwenyekiti wa Mtaa atakuwa Mwenyekiti wa mikutano yote ya kamati ya mtaa na Mkutano wa Hadhara, Msuluhishi wa migogoro midogomidogo ambayo haistahili kuitisha mikutano wa mtaa au kupeleka baraza la kata au Mahakama, kuwaongoza na kuwahimiza wakazi wa mtaa shughuli za maendeleo, kutekeleza kazi atakazopewa na kamati ya mtaa na Mkutano Mkuu wa Mtaa au kamati ya maendeleo ya kata na nyinginezo.

Aliongeza kuwa Wajibu wa Afisa Mtendaji wa Mtaa ni kuwa Mtendaji Mkuu wa Mtaa, kusimamia utekelezaji wa Sera za Halmashauri, kuishauri kamati ya maendeleo ya Mtaa kuhusu maendeleo ya Mtaa, kusimamia utekelezaji wa sheria ndogo  pamoja na sheria nyingine, kuishauri kamati ya mtaa kuhusu masuala ya ulinzi na usalama na nyinginezo. “Mrisho alibainisha.”

Kwa upande wake Inspekta wa Jeshi la Polisi Songea Melinda Mgumba kutoka  Dawati la jinsia na watoto ni sehemu maalmu  katika kituo cha Polisi inayoshughulikia Waaathirika wa vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia na watoto kwa lengo la kutenganisha sehemu ya huduma kwa waathirika wa ukatili na unyanyasaji wa kijinsia, kumpa muathirika nafasi ya kutulia itakayomfaa ili asiendelee kudhalilika, kusikiliza maelekezo kwa usiri mkubwa, kutoa ushauri kutegemea na lalamiko lililowasilishwa,  pamoja na kuchukua hatua.

Kwa upande wake Afisa Elimu Sekondari Janeth Moyo alisema Manispaa ya Songee imeweka Mkakati wa utoaji wa chakula shuleni katika kipindi cha mwaka 2023/2024 ikiwemo na kuitisha vikao vya wazazi na kufanya tathimini yay a uchangiaji wa michango ya mwaka mmoja  ambapo wazazi wameridhia kuchangia mahindi kilo 80 za Mahindi na Maharage kilo 24 na fedha shilingi 40,000 kwa ajili ya kuwezesha upatikanaji wa mahitaji mbalimbali pamoja na malipo ya wapishi.

Aliongeza kuwa kulingana na tathimini iliyofanyika kwa kipindi cha muhula wa kwanza wa masomo kuanzia januari 2023 hadi Mei 2023 takwimu zinaonesha ni 37% za wanafunzi  wa za Sekondari ndio wanaopta chakula cha mchana shulenia ambapo hupelekea kuwa na matokeo yakitaaluma  yasiyoridhisha.

IMEANDALIWA NA;                                                                                                                

AMINA PILLY;                                                                                                      

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.

                           










Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa