• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJILI SIKU YA MAADHIMISHO YA KICHAA CHA MBWA DUNIANI.

Tarehe ya kuwekwa: September 29th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema, amewataka wafugaji wa mbwa kufuata taratibu za ufugaji  ili kuepuka madhara ambayo yanaweza kutokea na kuathiri jamii kwa kung’atwa au kujeruhi watu au mifugo migine na kusababisha  jamii kupatwa na ugonjwa wa kichaa cha mbwa  ambao hauna  tiba  bali unakingwa  kwa chanjo.

Hayo yamebainishwa katika kilele cha maadhimisho ya siku ya kichaa cha mbwa duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo tarehe 28 septemba kila mwaka ambapo kwa Manispaa ya Songea iliadhimishwa katika uwanja wa Double ‘M’ uliopo kata ya Msamala Mtaa wa Mkuzo kwa lengo la  kutoa tathimini ya hatua zilizofikia katika kudhibiti kichaa cha mbwa na madhara yake.

Pololet alisema Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, Afya na Maliasili wanafanya jitihada katika kupunguza maambukizi ya kichaa cha mbwa kwa binadamu kwa kutoa mafunzo ya utunzaji bora wa mbwa kwa wafugaji wa mbwa na kuchukua hatua ya kuua mbwa kwa 50% wasio kuwa na wamiliki pamoja na kutoa chanjo ya mbwa.

 Aliongeza kuwa kila mfugaji  ahakikishe  anafungia mbwa wake kwenye banda au mnyororo kwa muda wote ili kuilinda jamii inayokuzunguka  na kuepuka madhara makubwa ikiwemo na kujeruhi watu, kusababisha hofu na kuwa tishio kwa jamii, kuchafua mazingira, kusambaza wadudu nyonya  na kueneza ugonjwa wa kichaa cha mbwa na tegu mbwa.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi  Manispaa ya Songea Philipo Beno Mpwessa amesema ili kudhibiti  au kutokomeza tatizo la kuzurula mbwa holela Halmashauri ya Manispaa ya Songea imeweka mikakati ikiwemo na kuratibu suala la mazingira kiutamaduni, kiuchumi, kijamii, kwa kuzingatia sheria, kanuni na haki za wanyama, kutoa elimu juu ya ufugaji bora na udhibiti wa magonjwa ya mbwa, kutoa chanjo ya kichaa cha mbwa, kuuwa mbwa wote wanaozurula na kutoza adhabu, kuwachukulia hatua wafugaji wote ambao hawajachanja mbwa wao,  kutenga fedha kwa ajili ya kudhibiti kichaa cha mbwa na kuhakikisha kila mfugaji wa mbwa kuhama na mbwa wake wakati anapohamisha makazi yake.

Beno alitoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassani kwa kuipa kipaumbele  wizara ya mifugo na uvuvi kwa kutoa fedha za kutosha kwa ajili ya kuwezesha upatikanaji wa chanjo ya kichaa kwa dozi 1000 ambayo imetolewa bure katika maadhimisho ya kichaa cha mbwa duniani.

Naye Dkt. Seria Shonyela  alisema mwaka 2021 Manispaa ya Songea walichanja mbwa 3960 na mwaka 2022 wanatarajia kutoa chanjo kwa mbwa 4000.

Kwa upande wa wafugaji wa mbwa waltoa shukrani kwa Serikali kuadhimisha siku ya kichaa cha ambapo imewasaidia kupata huduma ya chanjo bure bila malipo yoyte, pamoja na elimu ya ufugaji wa mbwa.

Kauli mbiu ya mwaka 2022 ni;     KICHAA CHA MBWA, AFYA MOJA, VIFO SIFURI ( RABIES, ONE HEALTH, ZERO DEATH)

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY.



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa