• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Yaliyojili Siku ya Maadhimisho ya UKIMWI Duniani Manispaa ya Songea

Tarehe ya kuwekwa: December 1st, 2022

Maadhimisho ya siku ya UKIMWI  Duniani huadhimishwa  kila ifikapo  tarehe mosi 1 desemba ya kila mwaka ambapo kwa Manispaa ya Songea Maadhimisho hayo yamefanyika kata ya Lizaboni.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema yaliyohudhuriwa na wadau mbalimbali wa ukimwi, Wataalamu na wananchi kwa lengo la  kuongeza ufahamu wa ugonjwa wa UKIMWI ambao unaosababishwa na Virusi vya UKIMWI.

Pololet alisema “ maadhimisho hayo yanalenga Kutoa fursa ya kutathmini hali halisi na mwelekeo wa kudhibiti Virusi vya UKIMWI (VVU) na UKIMWI kitaifa na kimataifa, Kutafakari changamoto, mafanikio na uimarishaji wa mikakati mbalimbali ya kudhibiti maambukizi ya VVU na UKIMWI.

Alibainisha kuwa maadhimisho yanasaidia Kutafakari na kutekeleza kauli mbiu inayotolewa kila mwaka kulingana na vipaumbele vya kidunia na kikanda na kitaifa kwa muktadha wa kitaifa pamoja na Kuwakumbuka watu wote waliopoteza maisha yao kutokana na UKIMWI pamoja na kuwajali yatima waliotokana na vifo vinavyohusiana na UKIMWI na  kuelimisha jamii kuhusu masuala ya unyanyapaa pamoja na kupinga na kukomesha kabisa vitendo na tabia za unyanyapaa kwa watu wanaoishi na Virusi Vya UKIMWI katika jamii.

Msisitizo mkubwa katika kauli mbiu hii inatukumbusha kuwa ‘’Binadamu wote ni sawa’’ hivyo mahitaji yetu sote ni sawa na tunahaki sawa kama binadamu, hivyo tunahitaji kuwa na mshikamano wa pamoja katika jamii kwenye kupinga kila aina ya viashiria vinavyokandamiza usawa na haki za binadamu pamoja na kuyafikia  makundi yote ya kijamii katika kuhakikisha huduma bora zinatolewa kwa wote nchini ili kuyafikia malengo ya 95 – 95 – 95 ifikapo mwaka 2025.

Naye Afisa Maendeleo ya jamii  Manispaa ya Songea Martin Mtani  alisema  Maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani hutoa fursa kote Duniani kutafakari kwa mara nyingine kuhusu tulipotoka, tulipo  na tunapokwenda katika mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI kwenye Halmashauri yetu na Taifa kwa ujumla.

Mtani alibainisha kuwa katika kipindi cha Julai 2021 hadi Juni 2022 Manispaa ya Songea  jumla ya watu 37856 wamepima afya zao, Wanaume 17273 na Wanawake 20585 kati hao Wanaume 611 na Wanawake 933 wamekutwa na maambukizi ya VVU sawa 4% wote wamefanikiwa kuunganishwa na huduma ya tiba na matunzo katika vituo vya kutolea huduma za VVU (CTC) ambapo hali halisi ya maambukizi inaonesha kushuka kwa 0.1% ikilinganishwa na mwaka wa fedha Julai 2020 hadi Juni 2021 ambapo ilikuwa ni 4.1%.

Ametoa wito kwa wananchi wote kuwa na tabia ya kupima na kutambua Afya zenu kwa hiyari kila mara endapo ukikutwa na maambukizi ya VVU unaunganishwa  katika huduma na tiba ya kufubaza VVU, kwa kufanya hivyo tutaimarisha afya zetu  na kuimarisha kinga za mwili dhidi ya magonjwa nyemelezi.

Aliongeza kuwa  ukipima na kujua huna maambukizi kunasaidia kuchukua tahadhari nakuacha tabia hatarishi zinazoweza kupelekea kupata maambukizi ya VVU.

kauli mbiu ya mwaka 2022 “Equality “imetafsiriwa kwa Kiswahili kuwa “Imarisha Usawa.”

 

Imeanadaliwa na;

Amina Pilly

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa