• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJILI UZINDUZI WA UNYWESHAJI WA DAWA ZA USUBI MANISPAA YA SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: September 23rd, 2022

Katibu Tawala Wilaya ya Songea Pendo Daniel amezindua zoezi la umezaji wa dawa tiba na kinga  dhidi ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ambalo hufanyika kuanzia tarehe 22 septemba hadi 24 septemba 2022 kwa kufanya sensa na kugwa dawa kwa  lengo la kudhibiti  dhidi ya magonjwa ya mabusha, Matende, Minyoo,  na kichocho.

Akiongea na waandishi wa Habari Ofisini kwake Bi pendo alisema kuwa ugonjwa wa USUBI ni ugonjwa  unaoenezwa na minyoo inayoitwa “ONCHOCERCA VOLVULUS” ni minyoo inayonezwa na inzi weusi wadogo wanaokaa kando kando ya mito ya maji yaendayo kwa kasi ambao husababisha ngozi kuwasha au kuwa na mabakamabaka meusi  mithili ya mamba au mjusi mweusi.

Alisema zoezi hilo la umezaji wa dawa za USUBI linafanyika katika Halmashauri zote 8 Mkoani Ruvuma ambapo kwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea zoezi litafanyika kwa siku 3 ambapo limeambatana na zoezi la semina elekezi kwa Wenyeviti wa mitaa 95, Watendaji wa kata 21, na wahudumu wa afya.

Ametoa rai kwa wananchi wote wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea  kujitokeza kwa wingi na kuhakikisha wanameza dawa hizo ambazo hazina madhara yoyote bali ni kinga ya upofu mto.

Kwa upande wake Mratibu wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Manispaa ya Songea Bload  Komba alisema “Uzindunduzi wa unyweshaji dawa kwa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa  wananchi 252282 ambao matarajio ni  kwa watu wasiopungua 201,830 sawa na asilimia 80% na watu ambao hawataruhusiwa kumeza dawa za usubi ni kwa watoto walio chini ya miaka 5, wamama wajawazito, na wagonjwa mahututi. Alibaisha.

Bload amewatoa hofu wananchi wote kuwa dawa za USUBI ni salama hazina madhara yoyote hata hivyo dawa hizo hutolewa kila mwaka kwa ajili ya kutibu na kudhibiti wa USUBI kwa kumeza dawa aina ya MECTZAN Kwa miaka kumi mfululizo.   

Kwa upande wa  wananchi Wakitoa ushuhuda mara baada ya kumeza dawa za Usubi  ambapo  walisema  kuwa dawa za usubi hazina madhara yoyote na  wametoa rai kwa  wananchi kuondoa hofu  juu ya dawa za USUBI  na kuthibitisha kuwa zinasaidia kuepukana na mangonjwa ya ngozi.   

 

Imeandaliwa na;

AMINA PILLY.


 



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bil. 22.9 Kujenga Masoko ya Kisasa Manzese A na B, na Kiwanda cha Kuchakata Mazao ya Nafaka Lilambo

    July 06, 2025
  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Tazama zote

Video

Makabidhiano ya Mkataba Soko la Manzese A&B
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa