• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJILI ZIARA YA RC RUVUMA AKITEMBELEA MIRADI MANISPAA YA SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: November 29th, 2022

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Kanal. Laban Thomas amewataka viongozi na wataalamu wa Manispaa ya Songea kukamilisha miradi ya ujenzi kwa wakati muafaka ili iweze kutumiwa na wananchi.

Hayo yamejili katika ziara ya Mkuu Mkoa wa Ruvuma iliyofanyika  tarehe 28 Novemba 2022 na kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo kwa lengo la kukagua hatua ya miradi   na kisha kuzungumza na watumishi wa Manispaa ya Songea.

Ziara hiyo imefanyika  kwa siku moja ambapo aliweza kutembelea  mradi wa ujenzi wa kituo cha afya Lilambo kinachojengwa kwa fedha za mapato ya ndani Mil. 514, ujenzi wa vyumba vya madarasa 6 katika shule ya  chandarua sekondari  fedha kutoka serikali kuu Mil. 120,  Ujenzi wa vyumba vya madarasa 6  Lizaboni sekondari  fedha kutoka Serikali kuu Mil. 120, kituo cha afya fedha kutoka  Grobal Fund Mil.545, pamoja na ujenzi wa madarasa mawili shule ya sekondari Matogoro kwa fedha kutoka Serikali kuu Mil. 40.

Kanal Laban alianza kwa kuwapongeza Manispaa ya Songea kwa kufanikisha kujenga  ujenzi wa kituo cha afya kilichopo kata ya Lilambo kilichojengwa kwa gharama ya Mil. 514 fedha kutoka mapato ya ndani ambapo ujenzi wake upo hatua ya ukamilishaji.

Amewataka wataalamu hao kushirikisha wananchi kila wanapotekeleza mradi kwenye kata husika ili kuleta uwazi na ushirikishwaji jamii ambao utaleta ulinzi shirikishi katika kulinda  rasilimali za umma ikiwemo kuundwa kwa kamati za ujenzi  ambazo zinajumuisha wanajamii.

Ametoa agizo kwa viongozi ngazi ya Wilaya na Halmashauri  kuwa na tabia ya kufanya ziara ya kutembelea miradi mingine inayotekelezwa ambayo sio miradi ya UVIKO au ya ujenzi wa madarasa iliyoanza kujengwa  hivi karibuni  ili kuleta msukumo wa kiutendaji  na kukamilisha kwa wakati.


Aidha, baada ya kukamilisha ziara hiyo, kiongozi alizungumza na watumishi wote wa Manispaa ya Songea ambapo aliwataka watumishi hao kusimamia miradi ya maendeleo kwa usahihi ili kutimiza wajibu na majukumu ya kazi kama mtumishi wa umma.

Ametoa Rai kwa idara ya Usafi wa Mazingira kutumia sheria ndogo za usafi wa mazingira kwa watakao kiuka sheria za usafi wa mazingira ili kuweka mji safi pamoja  na  upandaji wa  miti kwa kila kaya  ili kulinda miti ya awali ambayo ipo ndani ya mji.

 Akizungumzia kuhusu mahusiano kwa watumishi mahala pa kazi ambapo aliwataka wakuu   Idara na Vitengo kujenga mahusiano mazuri baina ya watumishi ambao ni wakuu wa idara na watumishi wa chini yake  ili kujenga uhusiana na uwajibikaji bora. “Kanal Laban amesisitiza".

Kanal. Laban amekemea vikali tabia ya baadhi ya watumishi ambao hukiuka taratibu za kiutumishi wa umma ambapo alitamka   nanukuu” ukipata ajira sio umepata utajiri na ukitafuta utajiri wakati ni mtumishi  wa umma unatafuta kutenda vitendo  ambavyo sio sahihi katika utendaji wa Serikali.” Mwisho wa kunukuu.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema alisema “ watumishi ndio injini ya maendeleo ya Halmashauri  na kila mmoja akitekeleza majukumu yake kupitia  idara husika kutakuwa na maendeleo yenye tija, na  endapo hatatekeleza kwa umakini  hakutakuwa na maendeleo,  hivyo amewataka watumishi hao kufanya kazi kwa weledi na kulinda maadili ya utumishi wa umma.

Naye Kaimu Mkurugenzi Manispaa ya Songea  Alto Liwolelu  alisema Halmashauri ya Manispaa ya Songea katika mwaka wa fedha 2022/2023 kwa kipindi cha mwezi Julai hadi October imepokea jumla ya Tshs 2,757,250,000.00 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya Elimu, Afya, Maendeleo ya Jamii na Utawala.

Imeandaliwa na;

AMINA PLYY

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.

 





Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa