• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJIRI BARAZA LA MADIWANI LA KUIDHINISHA MPANGO NA BAJETI 2023/2024

Tarehe ya kuwekwa: February 13th, 2023

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea  Mhe. Michael  Mbano amewataka viongozi  na wataalamu kuongeza ufanisi na weredi wa  kusimamia  zoezi  la ukusanyaji  wa  mapato ili  kufikia lengo la  makisio ya  Bajeti  iliyowekwa  kwa  mwaka  2023/2024

Hayo  yamejili  wakati  wa Baraza la Madiwani la kupitisha mapendekezo ya Rasimu ya Mpango na Bajeti  kwa mwaka 2023/2024  lililofanyika tarehe 09 Februari 2023 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea lililohudhuriwa na wadau mbalimbali,  wakuu wa  Idara na wananchi.

Mhe.  Mbano Alisema Nanukuu “ili  kufanikiwa lazima kuongeze  juhudi  ya kusimamia   ukusanyaji wa mapato kwa  kufanya  kazi kwa ushirikiano na wataalamu  ili kufanikiwa lengo la makusanyo ya  Bil. 5.6  kwa mwaka   2023/2024 ”Mwisho wa kunukuu"

Kwa upande wake  Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Dkt. Frederick Sagamiko alisema kuwa  mapendekezo ya Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2023/2024 iliyopitishwa itsaidia na kurahisisha utekelezaji wa shughuli mbalimbali ya maendeleo.

Aidha,  matarajio ya  Halmashauri  ya  Manispaa  ya  Songea ni kukusanya na kutumia Tsh Bil. 11.7 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbai ya maendeleo kutoka vyanzo mbalimbali kati ya fedha hizo kiasi cha Bil. 4,6 kutoka Serikali kuu, Waisani Bil. 5.3 na Halmashauri itachangia kutokana na mapato ya ndani kiasi cha Bil. 1.7 sawa na asilimia  40%.

Aliongeza  kuwa, Manispaa ya Songea imeomba kuidhinishiwa  kiasi cha Tsh Bil. 45.7 kwa ajili ya shughuli ya utekelezaji ambapo kati ya fedha hizo Bil. 30.2 Mishahara  na  Mil. 98.5 mengineyo, Luzuku ya Maendeleo kutoka Serikali kuu Bil.  8.9,  mapato ya ndani yanakisiwa  Bil. 5.6  ambapo  Bil. 34.4 iliombwa kuidhinishwa kati ya fedha hizo kiasi cha Bil. 31.1 Mishahara na Bil. 3.2 mengineyo.   

Kwa upande wake Katibu wa CCM Wilaya  ya Songea  Mjini Ndg. James Mgego amewataka viongozi na wataalamu  kuongeza uwajibikaji, uadilifu katika kusimamia ukusanyaji wa mapato ya Serikali pamoja na kufanya   ufuatiliaji wa   bajeti iliyowekwa iweze    kutatua  changamoto  za wananchi.(Alisisitiza)

Nao Waheshimiwa  Madiwani  walitoa pongezi zao kwa Wataalamu kwa kutenga bajeti ambayo imegusa kila sekta ambapo ni matarajio yao kuwa Rasimu ya Mpango na  Bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024   itasaidia kutatua changamoto  za  wananchi.(Walipongeza)

Imetolewa na;

AMINA PILLY

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.

 



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa