• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Yaliyojiri Siku ya Uzinduzi wa Dawa ya Usubi.

Tarehe ya kuwekwa: August 27th, 2021

Manispaa ya Songea imezindua rasmi zoezi la ugawaji dawa ya Usubi kwa kaya zote zilizopo ndani ya Manispaa ambapo ugonjwa huo ni miongoni mwa magonjwa yasiyopewa kipaumbele katika jamii ikiwemo na ugonjwa wa minyoo ya tumbo, matende, trakoma pamoja  na kichocho.

Uzinduzi huo umefanyika leo tarehe 27 Agosti 2021 katika ukumbi wa Mkuu wa Wilaya ya Songea na kuudhuriwa na Katibu tawala wa Wilaya ya Songea Pendo Daniel, wataalamu wa afya pamoja na waandishi wa habari.

Pendo amewataka wahudumu wa afya waliochaguliwa na kupewa mafunzo juu ya namna ya kusimamia zoezi la ugawaji dawa kuhakikisha wanamfikia kila mwananchi ndani ya Manispaa ya Songea pamoja na kufanya kazi hiyo kwa uweledi na uaminifu kama walivyoelekezwa ’Alisisitiza’.

Pia ametoa rai kwa wananchi wote kutumia dawa hizo ili kujikinga na ugonjwa wa Usubi lakini pia kuzingatia usafi wa mwili kwa ujumla, matumizi sahihi ya choo na usafi wa mazingira pamoja na kuachana na dhana potofu zinazopotosha jamii kuhusiana na dawa hizo.

Kwa upande wake mratibu wa kudhibiti magonjwa yasiyopewa kipaumbele Manispaa ya Songea Broad Komba amesema kuwa zoezi hilo la ugawaji dawa ya ugonjwa wa Usubi limeanza rasmi leo na linatarajiwa kumalizika tarehe 29 Agosti 2021.

Ameongeza kuwa dawa hizo zitatolewa kwa watu wote kwa kuzingatia kipimo maalumu cha urefu isipokuwa hazitatumika kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano, wakina mama wajawazito pamoja na wagonjwa mahututi.

Kwa mujibu wa tafiti za wataalamu wa afya, nchini Tanzania wananchi wote milioni 53 wapo hatarini kuambukizwa magonjwa haya yasiyopewa kipaumbele na idadi ya watu milioni 5 tayari wameshaathirika kwa mojawapo ya magonjwa hayo”Komba alibainisha”.

Ugonjwa huu wa Usubi husababishwa na minyoo inayoitwa “Onchocerca Volvulus” ambayo inaenezwa na inzi weusi wadogo wanaokaa kando ya mito yenye maji yaendayo kasi na husababisha ngozi kuwasha au kuwa na mabaka mabaka mithili ya mamba au mjusi pamoja na upofu.

NA AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

27.08.2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa