• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJIRI UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE

Tarehe ya kuwekwa: May 22nd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Songea  Wilman Kapenjama Ndile  amewataka Maafisa watendaji wa Kata  na Mitaa  kuhakikisha wanasimamia  kwa uthabiti  utekelezaji wa  Mkataba wa lishe ili upimaji wa  afua za Lishe uweze kufikia leo linakubaliwa.

“Alisema suala la chakula  kwa wanafunzi ni jukumu letu viongozi  hususani ngazi ya Halmashauri,  Kata/Mitaa,  shule pamoja na Wazazi wenye watoto  shuleni wahakikishe wanafunzi wote  wanapata chakula bora  kwa lengo la kuleta maendeleo mazuri katika afya ya akili, kimwili, kuimarisha kinga za mwili, na kuzuia magonjwa nyemelezi pia kupelekea kuongezeka  kwa kiwango cha ufaulu katika shule husika.”

Aidha, Wajibu wa  viongozi ni pamoja na kuijulisha  jamii kuwa, hali nzuri ya lishe inatokana na  ulaji  wa Mchanganyiko  kutoka makundi matano ya chakula na siyo chakula cha aina moja. “ Alibainisha”

Hayo yamejiri wakati wa kikao cha tathimini cha  utekelezaji wa Mkataba wa lishe  katika kipindi cha Januari hadi Machi 2024 kilichofanyika tarehe 21 Mei 2024 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea ambacho kilihudhuriwa na Maafisa Watendaji wa Kata pamoja na wakuu wa idara mbalimbali kwa lengo la kufanya mapitio ya utekelezaji wa afua za Lishe Manispaa ya Songea.

Akizungumza Katibu Tawala Wilaya ya Songea  Mtela Mwampamba  alisema “  Tunapoendelea  kuimarisha  Klabu za Lishe ni lazima tuhakikishe tunaimarisha  klabu hizo  kwa kufanya kazi kwa vitendo ikiwemo na uanzishaji wa bustani za lishe kwa shule za Msingi na Sekondari kwa lengo la kupata virutubisho vya lisho bora.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea  Adv.  Bashir Muhoja amewataka Maafisa watendaji wa Kata, Wakuu wa shule za Msingi na Sekondari wahakikishe wanasimamia uanzishaji wa bustani za mboga mboga na matunda kila shule, kuimarisha klabu za lishe na ushiriki wa wazazi katika kuhakikisha mtoto anapata chakula bora awapo shuleni, Pia ametoa wito kwa wazabuni wote wanaosambaza chakula shueni wahakikishe wanapeleka chakula chenye viini lishe.

Alisema elimu ya uzazi iendelee kutolewa kwa wazazi kabla ya kushika ujauzito wapewe elimu ya afya ya uzazi ili iwasaidie kufanya maamuzi sahihi ya kuzaa kwa umri ulio sahihi na kuzaa mtoto mwenye afya njema na mwenye uzito kamili.  “ Adv. Alisisitiza.”

Akiyataja mafanikio  ya jumla katika utekelezaji wa Mkataba wa lishe ni pamoja na kuongezeka kwa viwanda vinavyosindika unga wa mahindi na kuongeza viinilishe kutoka 71% hadi 77% kwa sasa, kuendelea kufanya SALIKI ya Kta na Mitaa kwa kuzingatia miongozo, kuongezeka kwa shule za Msingi na Sekondari ambazo wanafunzi wake hutumia unga ambao umeongezwa virutubisho ( Fortified maize flower) kutoka 5.8% hadi 10.9% kwa sasa, kuongezeka kwa wanafunzi wanaopata chakula  angalau fvfggggmlo mmoja wanapokuwa shuleni  kutoka 53% hadi  62.6% hadi sasa. Alibainisha.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa