• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJIRI ZIARA YA ALAT KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA.

Tarehe ya kuwekwa: December 5th, 2024

Mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Ruvuma, Mheshimiwa Kelvin Mapunda, amewataka Wataalamu wa Afya wa Hospitali ya Madaba Kuendelea Kutunza Miundombinu na Kutoa Huduma Bora kwa Wananchi

Kauli hiyo imetolewa na kiongozi huyo wakati wa ziara ya ALAT Mkoa wa Ruvuma, ambayo ilifanyika tarehe 4 Desemba 2024 ambapo ziara hiyo ilijumuisha ufuatiliaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwa ni pamoja na Hospitali ya Wilaya ya Madaba, ambapo viongozi hao walipata fursa ya kutathmini maendeleo ya miradi ya afya na miundombinu inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo.

Katika ziara hiyo, Mheshimiwa Mapunda alieleza umuhimu wa wataalamu wa afya katika kuhakikisha huduma za afya zinaendelea kwa ufanisi, huku wakizingatia na kutunza miundombinu ya hospitali ili kuhakikisha huduma zinapatikana kwa ufanisi zaidi.

 Aidha, alilipongeza taifa kwa jitihada zinazofanywa na Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan katika kuboresha miundombinu ya afya, elimu, maji, barabara, na huduma nyingine muhimu.


Akijibu baadhi ya changamoto zilizoainishwa katika taarifa iliyosomwa naMganga Mfawidhi wa Hospitali ya Madaba, Dkt. Chacha Wambura, Mheshimiwa Mapundaalisema kwamba Serikali inaendelea na jitihada za kuajiri watumishi wa sektambalimbali, hususan wataalamu wa afya, ili kukabiliana na changamoto yaupungufu wa wafanyakazi katika hospitali za umma ambapo alisisitiza kuwawananchi wanapaswa kuwa na subira wakati Serikali ikishughulikia changamotohizo kwa kadri inavyowezekana.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Madaba, Dkt. Chacha Wambura, alieleza kuwa hospitali hiyo ilianza kutoa huduma kwa wananchi mnamo tarehe 19 Septemba 2023, ikiwemo huduma za wagonjwa wa nje, kliniki ya baba, mama na mtoto, huduma za maabara, huduma za dharura na ajali, huduma za wagonjwa wa ndani, ustawi wa jamii na lishe, huduma za uzazi (kawaida na upasuaji), huduma za upasuaji mdogo, huduma ya kinywa na meno, pamoja na huduma ya kuhifadhi maiti.

Hata hivyo, alibainisha kuwa hospitali hiyo inakutana na changamoto  ya upungufu wa watumishi, ambapo mahitaji ya wafanyakazi ni 200, lakini hadi sasa watumishi waliopo ni watumishi 27 pekee.

Ziara hiyo ya ALAT Mkoa wa Ruvuma ilihudhuriwa na wajumbe wa jumuiya kutokahalmashauri zote za mkoa wa Ruvuma, wakiwemo wenyeviti wa halmashauri, naibumeya, na wakurugenzi kutoka halmashauri nane za mkoa huo.

Ziara hiyo ya ALAT Mkoa wa Ruvuma ilihudhuriwa na wajumbe wa jumuiya kutokahalmashauri zote za mkoa wa Ruvuma, wakiwemo wenyeviti wa halmashauri, naibumeya, na wakurugenzi kutoka halmashauri nane za mkoa huo.






Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa