• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJIRI ZIARA YA ALAT MKOA.

Tarehe ya kuwekwa: April 16th, 2024

NA;

AMINA PILLY – Mwandishi  wa ALAT Mkoa wa Ruvuma.

Jumuiya za Tawala za Serikali za Mitaa (ALAT)  Mkoa wa Ruvuma  wamefanya ziara ya kutembelea miradi ya Maendeleo katika Halmashauri  ya  Namtumbo  ambapo walitembelea mradi wa ujenzi wa madarasa mawili na matundu 6  ya vyoo uliopo katika kijiji cha Mkongo pamoja na Shule ya Sekondari ya wasichana ya Mkoa Dkt. Samia Suluhu Hassan .

Akizungumza Mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Ruvuma  Kelvin Mapunda alisema lengo la ziara  ni kutembelea miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Namtumbo, kujifunza na kupeana uzoefu wa uendeshaji wa shughuli za maendeleo.

Aidha, ameipongeza  Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha nyingi kwa ajili ya  uendeshaji wa miradi ya maendeleo  ikiwemo miundombinu  ya elimu, Afya na nyinginezo.  “Alipongeza”

Mhe. Mapunda amewapongeza wananchi wa kata ya Mkongo kwa kujenga madarasa  mawili  2  katika shule (shikizi) ya Mkongo ambayo imejengwa kwa gharama ya Mil. 26 kati ya hizo mil 20 ni nguvu za wananchi, na mil 6 ni fedha za mfuko wa jimbo.

Ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo kuhakikiksha wanakamilisha ujenzi wa madarasa hayo ili yaweze kupunguza mrundikano wa wanafunzi darasani,  pia itasaidia kupunguza umbali mrefu, pamoja na  kuchochea ongezeko la ufaulu kwa wanafunzi kutokana  kutokuwepo kwa utoro wa shule. “Alibainisha.”


Akizungumza  na wanafunzi wa shule ya Sekondari ya wasichana ya Mkoa ya  Dkt. Samia Suluhu Hassan iliyopo Wilayani humo ambapo amewataka wanafunzi hao kusoma kwa bidii, kuwa na nidhamu, utii na kumcha Mungu  katika kipindi chote cha masomo yao.

ziara  hiyo imefanyika kwa muda wa siku mbili  kuanzia tarehe  15 hadi 16 Aprili 2024  ambayo ilihudhuriwa na Wenyeviti wa Halmashauri 7,  Mstahiki Meya, Wakurugenzi wa Halmashauri 8, Waheshimiwa Madiwani 2 wawili kutoka kila Halmashauri pamoja na waandishi wa vikao wa Halmashauri.

Akisoma taarifa Mwl Dafrosa Chilumba Mkuu wa shule ya wasichana ya Mkoa  Dkt. Samia Suluhu Hassan  alisema  awamu ya kwanza Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa Dkt. Samia  Suluhu Hassan ilipokea fedha  kiasi  cha Tsh  3,000,000,000  kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 12, mabweni 5, maabara 4, jengo la utawala 1, nyumba ya walimu 2 moja, nyumba ya matroni 1, vyoo  matundu 16,  pamoja na  Bwalo 1 na ujenzi umekamilika.

Awamu ya pili Shule ilipokea Bil. 1,100,000,000 kwa ajili ya ujenzi  wa madarasa  10, jengo la TEHAMA 1, maktaba 1, nyumba 2 za  walimu  2,  nyumba ya vyumba 3 moja, pamoja na mabweni 4 ambapo baadhi ya miradi imekamilika na miradi mingine  ipo hatua ya ukamilishaji.  “Alibainisha.”


Kwa  upande wa wanafunzi wa shule ya wasichana  ya Mkoa  Dkt. Samia Suluhu Hassan wametoa shukrani kwa Serikali kwa kujenga shule ya Wasichana ya Mkoa ambayo itawezesha kusoma katika mazingira mazuri na wameaahidi kufanya vizuri katika masomo yao.

"MWISHO."

.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa